Ruto avunja baraza la mawaziri Kenya

July 11, 2024 12:54 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Asema shughuli zote za Serikali zitaratibiwa na Katibu Mkuu wakati mchakato wa kupata baraza jipya ukiendelea.

Dar es Salaam. Rais wa Kenya William Ruto amevunja baraza la Mawaziri pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali leo Julai 11, 2024.

Ruto ametangaza kuwafuta kazi viongozi hao wakati akihutubia Taifa kupita televisheni ambapo amesema kuwa uamuzi huo umefanyika baada ya kufanya tathmini ya kina.

“Baada ya kutafakari, kusikiliza kwa makini kile watu wa Kenya walisema na baada ya tathmini ya kina ya utendaji wa Baraza langu la Mawaziri na mafanikio na changamoto zake, ninayo, kwa mujibu wa mamlaka niliyopewa na Ibara ya 152(1) na 152(5)(b) ya Katiba Kifungu cha 12 cha Katiba. Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, nimeamua kuwafuta kazi mara moja Makatibu wote wa Baraza la Mawaziri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kutoka Baraza la Mawaziri la Jamhuri ya Kenya isipokuwa Waziri Mkuu na Waziri wa Masuala ya Nje na Diaspora,” alisema Rais Ruto.

Huenda huu ni muendelezo wa maboresho ya Serikali ya kiongozi hiyo kufuatia maandano ya vijana maarufu kama Gen Z yaliyofanyika kwa wiki kadhaa nchini humo.

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW