Robert Mugabe afariki dunia

September 6, 2019 4:41 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Rais wa zamani wa Zimbabwe, Robert Mugabe amefariki dunia akiwa nchini Singapore ambako alikuwa anapatiwa matibabu kwa muda mrefu sasa. 

Rais wa sasa wa nchi hiyo, Emmerson Mnangagwa amethibitisha kutokea kwa kifo cha Mugabe aliyefariki akiwa na umri wa miaka 95 kupitia ukurasa wake waTwitter. 

Amesema Mugabe alikuwa alama ya ukombozi, mtu wa Kiafrika aliyejitolea maisha yake kwa ukombozi na uwezeshaji wa watu wake. 

“Mchango wake katika historia ya Taifa letu na bara kamwe hautasahaulika. Nafsi yake ipumzike kwa amani ya milele!,” ameandika Rais Mnangagwa katika ukurasa wake wa Twitter,

Mugabe alikuwa moja wa viongozi wa Afrika waliokaa madarakani muda mrefu. Ameiongoza Zimbabwe kutoka 1980 mpaka 2017, alipoondolewa madarakani na makamo wake kwa msaada wa jeshi.

Alizaliwa Februari 21, 924 nchini Zimbabwe. Atakumbukwa zaidi kwa uanamapinduzi wake ulioiwezesha #Zimbabwe kupata uhuru kutoka kwa Uingereza. 

Ameacha mjane, Grace Mugabe, na watoto watatu; Bona Mugabe, Chatunga Bellarmine Mugabe, Robert Peter Mugabe Jr.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
16 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Nukta TV

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Nukta TV

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV