Serikali kushusha tozo maendeleo ya ufundi (SDL)
June 11, 2020 2:23 pm ·
Mwandishi
- Zimeshushwa kutoka asilimia 4.5 hadi asilimia 4 ili kuwapunguzia waajiri mzigo na gharama za uendeshaji.
- Kwa muda mrefu waajiri wamekuwa wakilalamikia uwepo wa kiwango kikubwa cha tozo hizo ambazo huathiri pia mapato yao.
Dar es Salaam. Serikali imependekeza kushusha kiwango cha tozo kwa ajili ya maendeleo ya ufundi stadi (Skills Development Levy) kutoka asilimia 4.5 hadi asilimia 4 ili kuwapunguzia waajiri mzigo na gharama za uendeshaji.
Waziri wa Fedha na Mipango Dk Philip Mpango amesema hatua hiyo inatarajiwa kupunguza mapato ya Serikali kwa kiasi cha Sh42.07 bilioni.
“Lengo la marekebisho haya ni kuwapunguzia waajiri mzigo na gharama za uendeshaji wa shughuli zao na kutimiza azma ya kupunguza tozo hizi hatua kwa hatua bila kuathiri mapato kwa kiasi kikubwa,” amesema Dk Mpango.
Kwa muda mrefu waajiri wamekuwa wakilalamikia uwepo wa kiwango kikubwa cha tozo hizo ambazo huathiri pia mapato yao.
Latest
7 hours ago
·
Fatuma Hussein
Bima ya Afya kwa Wote kuanza rasmi Januari 26
8 hours ago
·
Kelvin Makwinya
Mwigulu azindua kituo cha uokoaji Mwanza, asisitiza uwajibikaji
8 hours ago
·
Imani Henrick
Kutoka NIDA hadi Jamii Namba: Safari ya utambulisho wa kidijitali Tanzania
10 hours ago
·
Fatuma Hussein
Edwin Mtei: Mwasisi wa BoT, Chadema anayekumbukwa kwa mengi