Jumatatu, Julai 08, 2024
Dar es Salaam. Rais John Magufuli amemteua Dk Leonard Chamriho kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya ushauri wa uwekezaji wa mapato ya mafuta na gesi.
Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, imeeleza kuwa uteuzi huo wa Dk Chamriho ni Katibu Mkuu wa Uchukuzi katika Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, umeanza leo (Septemba 25, 2019).
Rais Magufuli amewateua pia Wajumbe wanne wa Bodi hiyo.
U T E U Z I. pic.twitter.com/xJpyz0SPxo
— Gerson Msigwa (@MsigwaGerson) September 26, 2019