Rasmi: Apple kuisambaratisha iTunes

June 5, 2019 7:09 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link

Apple inamaliza minong’ono iliyokuwepo juu ya mpango wa kampuni hiyo kubwa duniani kuivunja huduma hiyo hasa baada ya kuwepo ushindani mkali katika tasnia hiyo. Picha|Mtandao.


  • Kwa sasa iTunes itagawanywa katika programu tumishi (Apps) tatu za video, muziki na muziki wa mtandaoni.  
  • Apple inahamia kuelekea kuwa mtoa huduma wa burudani mbalimbali, badala ya kuwa mtoa huduma wa vifaa vya kielektroniki pekee.
  • Nafasi ya iTune itachukuliwa na programu nyingine ya  MacOS Catalina.

Watumiaji huduma za iTunes kupata muziki, sasa wajiandae kuanza kutumia huduma tofauti na waliozoea baada ya iTunes kuvunjwa na kihitimisha safari ya miaka 18 ya kuwepo sokoni na kuwatoa wengi katika ulimwengu wa muziki.

Kampuni ya Apple ya Marekani inayotengeneza simu za Iphone imetangaza kuivunja programu yake tumishi ya iTunes iliyokuwa inatumika kama soko la muziki la mtandaoni katika mkutano uliofanyika California, Marekani hivi karibuni. 

Nafasi ya programu hiyo itachukuliwa na programu nyingine ya  MacOS Catalina ambayo Apple imeitambulisha tayari ambapo kwa sasa iTunes itagawanywa katika programu tumishi (Apps) tatu za video, muziki na muziki wa mtandaoni.  

Ina maana watumiaji wanaweza kutarajia programu mpya ya muziki ili kutoa kile ambacho iTunes hufanya sasa, lakini kwa interface (muonekano) bora.


Soma zaidi: 


Kwa kutenganisha huduma zake, Apple inahamia kuelekea kuwa mtoa huduma wa burudani mbalimbali, badala ya kuwa mtoa huduma wa vifaa vya kielektroniki pekee.

Taarifa hiyo ya Apple inamaliza minong’ono iliyokuwepo juu ya mpango wa kampuni hiyo kubwa duniani kuivunja huduma hiyo hasa baada ya kuwepo ushindani mkali katika tasnia hiyo.

Ujio wa huduma za muziki mtandaoni kama Tidal na Spotify ulishusha pia umaarufu wa huduma za iTunes na huenda mpango mpya wa Apple ukaisaidia kuongeza mapato katika nyanja hizo na kuimarisha ushindani.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.