Rais Samia azindua miradi ya maendeleo ziarani Tanga

February 24, 2025 7:13 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni pamoja na uzinduzi wa jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Bumbuli pamoja na uwekwaji wa jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa bwawa la Mkomazi.

Dar es Salaam, Rais Samia Suluhu Hassan amezindua jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Bumbuli pamoja na kuweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa bwawa la Mkomazi unaotajwa kuchochea kilimo jijini Tanga.

Rais Samia ambaye yuko ziarani kwa wiki moja jijini humo leo Februari 24, 2025 ametembelea maeneo mbalimbali ikiwemo Bumbuli, Lushoto na Korogwe akizungumza na wananchi pamoja na kuzindua miradi hiyo.

Akizungumza baada ya kuzindua bwawa la Mkomazi Rais Samia amesema “Lengo letu mabwawa haya yatumike kwa kilimo, yatumike kwa mambo mengine pia lakini kubwa ni uzalishaji wa mazao ya kilimo… tunakwenda kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kilimo, Mwalimu Nyerere alisema kilimo ndiyo uti wa mgongo wa taifa letu, tunakwenda kulithibitisha hilo”

Mradi wa ujenzi wa bwawa la Mkomazi unaotajwa kuchochea kilimo jijini Tanga. Picha | Global Publishers

Kwa mujibu wa Mhandisi wa Umwagiliaji Mkoa wa Tanga, Leonard Someke, bwawa hilo lina ukubwa wa hekta 1,469 na uwezo wa kuhifadhi lita za ujazo bilioni 17.5 za maji.

Bwawa hilo linatarajiwa kutumika kwa umwagiliaji wa hekta 9,000 katika vijiji 29 vya Wilaya ya Korogwe, hivyo kuongeza uzalishaji wa mazao na kuinua kipato cha wakulima wa eneo hilo.

Mpaka sasa ujenzi wa Bwawa hilo umefikia asilimia 30 na linatarajiwa kukamilika baada ya miezi 18 huku likitarajiwa kuleta tumaini jipya kwa wakulima wa eneo hilo likiwahamisha kutoka kilimo cha kutegemea mvua hadi kilimo cha umwagiliaji.

Rais Samia pia amezindua jengo jipya la Halmashauri ya Wilaya ya Bumbuli, akisisitiza umuhimu wa miundombinu bora kwa watumishi wa umma na wananchi. 

Uzinduzi wa jengo la Halmashauri unaonyesha umuhimu wa miundombinu bora kwa watumishi wa umma na wananchi. Picha | Habari leo.

“Jengo hili ni la wananchi wa Bumbuli. Huduma zote zitapatikana hapa, na naomba mlitumie kwa manufaa yenu. Lengo letu ni kuboresha huduma kwa wananchi na kutoa fursa kwa watumishi wetu kufanya kazi zao kwa ufanisi,” amesema Rais Samia.

Changamoto ya barabara, wanyama pori kutatuliwa

Aidha, Rais Samia ametumia ziara hiyo kusikiliza changamoto za wakazi wa wilaya ya Bumbuli na Lushoto ikiwemo wanyamapori kuharibu mazao ya wakulima.

“Nataka nimuagize Waziri wa Utalii aone uwezekano wa kufanya mapitio ya kanuni za fidia kwa wale ambao wanaingiliwa kwenye mashamba yao,” amesema Rais Samia.

Rais Samia pia ameweka wazi hatua za kuboresha miundombinu ya barabara katika mkoa wa Tanga. Amesema tayari serikali imetenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Soni–Bumbuli–Korogwe pamoja na barabara ya Tanga–Bagamoyo kupitia Pangani. 

“Nataka niwaambie tarehe sita mwezi ujao tunafungua tenda kutafuta mkandarasi na barabara itaanza kujengwa,” alitangaza Rais Samia.

Barabara hiyo itajengwa kwa urefu wa kilomita 22 kutoka Soni kuelekea Bumbuli, na kilomita 9.3 kutoka Kwa Meta hadi Kwa Shemsi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV