Rais Samia ateua Naibu Kamishna Mkuu TRA

January 18, 2022 7:09 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Amemteua Mcha Hassan Mcha kuwa Naibu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Mcha Hassan Mcha kuwa Naibu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais- Ikulu, Jaffar Haniu katika taarifa yake iliyotolewa leo Januari 18, 2022 amesema kuwa Mcha anachukua nafasi ya Msafiri Lameck Mbibo ambaye ameteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Madini.

Kabla ya uteuzi huo Mcha alikuwa Kamishna wa Udhibiti na Utekelezaji (Control and Enforcement) Makao Makuu ya TRA.

Pia, taarifa hiyo imesema kuwa Rais Samia amemteua Balozi Celestine Joseph Mushy kuwa Balozi wa Tanzania nchini Austria.

Balozi Muhy alikuwa Katibu Tawala Msaidizi, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV