Rais Samia atengua uteuzi wa Mkuu wa Mkoa Simiyu, Mkuu wa Wilaya Nanyumbu.

June 11, 2024 7:50 am · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Amteua Kenan Kihongosi kuwa Mkuu wa Mkoa Simiyu.
  • Uapisho wa viongozi wateule kufanyika baadae.

Dar es Salaam. Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameendelea kufanya panga pangua ya viongozi wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, awamu hii akitengua uteuzi wa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Dk. Yahaya Nawanda na Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu mkoani Mtwara Dk. Stephen Isaac Mwakajumulo.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu leo Juni 11, 2024 imebainisha kuwa Rais Samia amemteua Kenan Laban Kihongosi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu akichukua nafasi ya Dk. Yahaya Ismail Nawanda ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Kabla ya uteuzi huo Kihongosi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Momba mkoani Songwe ambapo alihamishiwa kushika nafasi iliyoachwa wazi na Fakii Raphael Lulandala aliyeteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM).

Hata hivyo, taarifa ya utenguzi wa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu inakuja wakati ambao kumekuwepo na mijadala kumhusu kiongozi huyo kujihusisha na vitendo vya ukatili wa kijinsia hususan katika mitandao ya kijamii.

Utenguzi huo unakuja ikiwa imepita siku nne tu tangu Rais Samia alipofanya mabadiliko ya viongozi kwenye nafasi mbalimbali za wizara, pamoja na Tamisemi kwa kile kilichodaiwa kuboresha utendaji kazi serikalini.

Taarifa hiyo imeongeza kuwa Rais Samia amemteua Elias Daniel Mwandobo kuwa Mkuu wa Wilaya ya Momba ambapo kabla ya uteuzi huo Mwandobo alikuwa Afisa Mwandamizi, Ofisi ya Rais Ikulu.

Wengine walioteuliwa ni pamoja na Christopher Magala, aliyeteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu akichukua nafasi ya Dk. Stephen Isaac Mwakajumilo ambaye uteuzi wake umetenguliwa na George Hillary Herbert ambaye ameteuliwa kuwa Msajili wa Mahakama ya Rufani.

“Uapisho wa Mkuu wa Mkoa na Msajili wa Mahakama ya Rufani utafanyika kwa tarehe itakayopangwa baadaye,” imebainisha taarifa hiyo.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia azindua minara 758, aacha maagizo mazito juu ya mkongo wa taifa

Rais Samia azindua minara 758, aacha maagizo mazito juu ya mkongo wa taifa

Nukta TV

JAJI MKUU: Njia za asili ni mojawapo ya njia halali za utatuzi wa migogoro

JAJI MKUU: Njia za asili ni mojawapo ya njia halali za utatuzi wa migogoro

Nukta TV

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Nukta TV