Rais Samia amtaka Dk Mwigulu kutekeleza majukumu ya Serikali kwa kasi

November 14, 2025 1:15 pm · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link
  • Majukumu hayo ni yale yaliyoainishwa katika ilani ya uchaguzi ya CCM.

Arusha. Rais wa Tanzania Samia Suluhu amemuapisha Waziri Mkuu Mteule Dk Mwigulu Nchemba na kumuagiza kusimamia utekelezaji wa majukumu ya Serikali kwa kasi kubwa ndani ya miaka mitano ijayo.

Rais Samia ametoa maagizo hayo leo Novemba 14, 2025 katika hafla ya kumuapisha Dk Mwigulu Nchemba iliyofanyika Chamwino, Dodoma akibainisha kuwa muda wa miaka mitano uliopo ni mchache kulinganisha na ahadi walizoziahidi katika ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) hivyo hana budi kutekekeza majukumu hayo kwa kasi kubwa.

“Hatuna budi kuongeza kasi katika utendaji wetu, utakwenda kusimamia Baraza la Mawaziri ambao nao wanaongoza sekta tofauti tofauti, ni wajibu wako kuhakikisha kasi ya utekelezaji wa yale tuliyoyapanga inaongezwa ili tuweze kuyatekeleza yote ndani ya muda mfupi,”amesema Rais Samia.

Maelekezo hayo ya Rais Samia yanaenda sambamba na ahadi ya waziri mkuu huyo mpya wakati akihutubia kwa mara ya kwanza mara tu baada ya kuthibitishwa na Bunge kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania akiahidi kutumika kukidhi mahitaji ya Watanzania.

“Watumishi wa umma na Watanzania sote kwa ujumla lazima twende na spidi ya kupandia mlima, twende na gia ya kupita kwenye mawimbi, twende na gia ya kupita kwenye anga lenye mawingu, lazima chombo kifike salama na watu wake wafike salama,”lisema Dk Mwigulu Novemba 13,2025 Bungeni Dodoma.

Pamoja na hayo Rais Samia amemtaka Dk Nchemba kutekeleza majukumu yake kwa weledi kuepuka vishawishi kutoka kwa ndugu jamaa na marafiki akibaonisha kuwa uteuzi wake ulikuwa na ushindiani mkubwa.

“Uteuzi  wako umepitia ushindani mkubwa na katika vigezo kadhaa, umeibuka na vigezo vingi kidogo kuliko wengine ulioshindana nao n vigezo vyote tumepima maeneo mbalimbali ya nchi yetu kubwa zaidi ni kuwatumikia Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania…

…Kwa umri wako mzigo huu ni mkubwa, kwa umri wako vishawishi ni vingi vya marafiki ndugu, jamaa, nafasi yako ile haina rafiki, hina ndugu, haina jamaa ni nafasi ya kulitumikia Taifa la Tanzania,” amesisitiza Rais Samia.

Kwa uapisho huo Dk Mwigulu ambaye pia amewahi kuwa Waziri wa Fedha kwa awamu mbili zilizopita anakuwa Waziri Mkuu wa 12 akichukua nafasi ya Kassim Majaliwa aliyehudumu nafasi hiyo kwa miaka 10 iliyopita chini ya Rais wa awamu ya tano John Pombe Magufuli na baadae Rais Samia Suluhu baada ya mtangulizi wake kupoteza maisha.

/
No matches found for this filter
22 May, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
23 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
23 May, 2026
No active movers today
Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MIKOA YA KIPOLISI ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI TANZANIA BARA 2025

MIKOA YA KIPOLISI ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI TANZANIA BARA 2025

Nukta TV

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

Nukta TV

MIKOA 5 ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI 2025 TANZANIA BARA

MIKOA 5 ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI 2025 TANZANIA BARA

Nukta TV