Rais Samia afanya uteuzi

December 23, 2021 2:51 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Amemteua Profesa Othman Chande Othman kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TBS.
  • Amemteua Dk Kalimwage Mlimuka kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Ushindani (FCC).

Dar es Salaam. Huenda sikukuu za mwisho wa mwaka zikawa chungu na tabasamu kwa baadhi ya viongozi wa taasisi mbalimbali za Serikali baada Rais Samia Suluhu Hassan kufanya mabadiliko katika taasisi hizo.

Rais Samia amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali akiwemo Profesa Othman Chande Othman kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS).

Prof Othman ambaye alikuwa Mhadhiri mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) anachukua nafasi ya Dk Fenella Mukangara ambaye uteuzi wake umetenguliwa. 

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Jaffar Haniu katika taarifa yake iliyotolewa leo Desemba 23, 2021 amesema pia Rais Samia amemteua Dk Kalimwage Mlimuka kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Ushindani (FCC).

“Dk Mlimuka anachukua nafasi ya Prof Humphrey Moshi aliyemaliza muda wake. Dk Mlimuka ni Mkurugenzi Mstaafu wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE),” amesema Haniu katika taarifa hiyo.

Aidha, Dk Andrew Kutua ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi ya Taifa ya Utafiti ya Magonjwa ya Binadamu (NIMR) akichukua nafasi ya Dk Deudatus Mtasiwa ambaye amemaliza muda wake.

Uteuzi huo umeanza leo Desemba 23, 2021.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV