Rais Magufuli ateua bosi mpya taasisi ya elimu ya watu wazima

February 20, 2019 10:06 pm · Daniel
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni mtaalamu wa masuala ya elimu Dk Michael  Ngu’mbi aliyekuwa akihudumu Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT).
  • Bosi huyo anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dk Fidelice Mafumiko aliyeteuliwa kuwa Mkemia Mkuu wa Serikali.

Dar es Salaam. Taasisi ya Elimu ya Watu  Wazima(TEWW) imempata bosi mpya baada ya Rais John Magufuli kumteua Dk Michael  Ngu’mbi kuwa mkurugenzi wa taasisi hiyo inayotoa elimu kwa watu wazima na ambao hawakubahatika kupata elimu katika mfumo rasmi wa kielimu.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi  wa Mawasiliano ya Rais Ikulu  Gerson Msigwa leo (20 Februari mwaka 2019) inaeleza Dk Ngu’mbi anachakua nafasi ya Dk Fidelice Mafumiko ambaye ameteuliwa kuwa Mkemia Mkuu wa Serikali.

Dk Ng’umbi ni mtaalamu wa masuala ya elimu aliyejipatia shahada yake ya uzamivu kutoka Chuo Kikuu cha Reading nchini Uingereza.

Kabla ya uteuzi huo  Dk Ng’umbi alikuwa Mhadhiri Mwandamizi Kitivo cha Elimu Cha Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (Opean Univestity of Tanzania ).

Uteuzi wa Ng’umbi ni mwendelezo wa Rais Magufuli kuteua wasomi kutoka vyuo vikuu nchini katika kuongoza taasisi mbalimbali za umma wakiwemo Katibu Mkuu Wizara ya Maji Profesa Kitila Mkumbo , Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi na Profesa Shukran Manya waliokuwa wakifundisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Katika uteuzi huo uliotangazwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi, Rais Magufuli pia amemteua Jaji Stephen Magoiga kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Ushindani (Fair Competition Tribunal – FCT). Jaji Magoiga amechukua nafasi ya Jaji Barke Mbaraka Sehel ambaye ameteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani. 

Taarifa hiyo ya Ikulu imeleza uteuzi huo wa viongozi umeanza Februaria 19, 2019.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
21 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
21 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Nukta TV

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Nukta TV

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

Nukta TV