Rais Magufuli amkaribisha Putin Tanzania

March 14, 2019 8:27 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link

Rais John Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na ujunbe wa Urusi ulioongozwa na mjumbe maalum wa Rais wa Urusi Vladimir Putin katika masuala Afrika ambaye ni Naibu Waziri wa Mambo Nje, Mikhail Bogdanov leo (Machi 13, 2019) Picha| lkulu Jijini Dar es Salaam.


  • Amemkaribisha na wawekezaji wa nchi hiyo kutembelea nchiini ili kuwekeza katika fursa mbalimbali zilizopo.
  • Dk Magufuli amesema Tanzania inatambua umuhimu wa ushirikiano na Urusi itakuza na kuendeleza uhusiano katika masuala ya biashara, uwekezaji, utalii na utoaji wa huduma za kijamii ikiwemo afya, elimu na miundombinu. 

Dar es Salaam. Rais John Magufuli amemkaribisha Rais wa Urusi Vladimir Putin na wawekezaji wa nchi hiyo kutembelea Tanzania ili kuwekeza katika fursa mbalimbali zilizopo nchini. 

Amesema Tanzania inatambua umuhimu wa ushirikiano uliopo kati yake na Urusi ina itaendeleza na kuimarisha katika masuala ya biashara, uwekezaji, utalii na utoaji wa huduma za kijamii ikiwemo afya, elimu na miundombinu. 

Taarifa kutoka Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imeeleza mara baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa Urusi ulioongozwa na mjumbe maalum wa Rais Putin katika masuala Afrika ambaye ni Naibu Waziri wa Mambo Nje, Mikhail Bogdanov leo (Machi 13, 2019) lkulu Jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli amesema Watanzania wanaipenda Urusi na anamkaribisha rais huyo atembelee Tanzania.

“Naomba ufikishe ujumbe wangu kwa Rais Putin kuwa Watanzania wanaipenda Urusi na tunamkaribisha kuja kutembelea nchi yetu pamoja na wananchi wengine wa Urusi, tunawakaribisha pia wawekezaji waje wawekeza katika fursa mbalimbali zilizopo hapa Tanzania kwa manufaa yetu sote,” amesema Rais Magufuli katika taarifa iliyosainiwa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu. 

Naye Bogdanov, ambaye amewahi kutembelea Tanzania miaka nane iliyopita, ameipongeza Serikali kwa kasi nzuri ya maendeleo iliyopata katika kipindi kifupi na amebainisha kuwa Urusi imedhamiria kukuza zaidi uhusiano na ushirikiano mzuri uliopo kati yake na Tanzania.


Soma zaidi: Magufuli aangazi rada kuongeza mapato Tanzania


Amesema Urusi ina mpango mahususi wa kushirikiana na nchi za Afrika ikiwemo Tanzania katika kuongeza kasi ya maendeleo na kuwa hivi karibu Tanzania na Urusi zitatiliana saini makubaliano ya kuanzisha tume ya pamoja ya ushirikiano (WM Permanent Commission-JPC) katika biashara, uwekezaji na uchumi ili rasilimali na fursa zilizopo katika pande zote zitumike kwa manufaa wananchi wa nchi hizo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi amesema tume hiyo itakayoanzishwa itasaidia  kukuza uchumi kupitia madini, gesi na utalii hasa wakati huu ambapo Urusi imeitazama Tanzania kuwa nchi yenye vivutio bora vya utalii duniani.

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...