Pilipili ya nanasi: Maandalizi hadi kuitumia kwa chakula

October 21, 2022 4:32 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link

Pilipili ni kiungo muhimu chenye kuongeza ladha na hamu ya kula (appetite) kwenye chakula.

Kumekuwa na ubunifu mbalimbali unaofanyika kwenye kiungo hicho kuhakikisha kinakuwa na ladha tofauti tofauti kuendana na haja ya mlaji.

Aina ya pilipili inayozungumziwa hapa ni ile inazosagwa na kuwa katika hali ya kimiminika. Inaweza kuwa ya ladha ya embe, limao, ukwaju, ubuyu na nyingine nyingi.

Leo tujifunze jinsi ya kutengeneza pilipili yenye ladha ya nanasi.

Maandalizi

Hatua ya kwanza baada ya kununua mahitaji ya aina hii ya pilipili ni kuosha na kumenya nanasi. Kama unatengeneza kiasi kidogo cha pilipili unaweza kununua vipande vya nanasi vinavyouzwa vikiwa vimeshakatwa katwa.

Tutatumia vipande vichache vya nanasi ili utamu wa tunda hilo usizidi kiasi cha pilipili ulizonazo.

Mimi leo nimetumia vipande viwili vya nanasi huku kwetu vinauzwa Sh1,000.

Ukimaliza kuandaa nanasi osha, menya na ukatekate nyanya, kitunguu, karoti hoho kwa saizi kubwa kiasi. 

Washa jiko na uvichemshe kwa dakika tano kisha uache vipoe.

Vikipoa weka vipande vya nanasi, nyanya, karoti, hoho, kitunguu na pilipili kwenye blenda na usage mpaka vilainike.

Ukimaliza kusaga weka mchanganyiko kwenye sufuria yenye mafuta kiasi kulingana na wingi wa pilipili yako kisha uache uchemke.

Ukichemka mimina mchanganyiko wako kenye sufuria. Ongeza  maji kiasi ili mchanganyiko wako usiwe mzito sana.

Baada ya hapo ongeza chumvi, maji ya limao na kiungo cha mchuzi kama unapendelea.

Baada ya hapo pilipili yako itakuwa tayari unaweza kuiweka kwenye chupa za plastiki kwa ajili ya kuuza  au kwa matumizi ya nyumbani.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV