Jinsi ya kupika kitimoto nazi

August 30, 2023 1:14 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni pishi jipya, hivyo halipatikani sehemu nyingi
  • Inasaidia kuongeza ubunifu kwa wauzaji wa nyama hiyo
  • Ni rahisi kuandaa na unaweza kupika nyumbani 

Nyama ya nguruwe ni miongoni mwa vitoweo vitamu na vyenye walaji wengi duniani kote ambapo kwa hapa nchini Tanzania inafahamika zaidi kwa jina la kitimoto.

Hakuna ushahidi rasmi juu ya maana na historia ya jina hilo ila baadhi ya walaji wa nyama hiyo husema, lilitokana na ukweli kwamba nyama hiyo ikiwa ya moto inakuwa tamu zaidi.

Ni ukweli ulio bayana kuwa utamu wa nyama hii ndiyo unafanya watu wengi kuvutiwa nayo huku watu wengine wakiongeza manjonjo na ubunifu zaidi, ili kuongeza utamu wakati wa kuiandaa hapo utakutana na kitimoto choma, kitimoto rosti, makange na nyingine nyingi.

Kitimoto nazi ni pishi jipya

Aina zote hizo zimezoeleka sana, hauhitaji kueleza maneno mengi kwa wauzaji wakati wa kuagiza, ila kuna hii aina mpya ya upishi wa rosti ya kitimoto ambayo inaungwa nazi, leo ningependa tujifunze kwa pamoja.

Ukiwa kama mpishi unayetamani kuongeza ujuzi huu katika kijiwe chako cha kuuzia kitimoto au unatamani kupika nyumbani kwa ajili ya familia, upo mahali sahihi fuatana nami mpaka pale mapishi ya kitimoto nazi yatakapokamilika.

Tuingie Jikoni

Mapishi ya kitimoto rosti kama ilivyo aina nyingine ya nyama huanza kwa kuchemsha nyama ambayo utaikatakata vizuri utaisafisha na kuiwekea viungo upendavyo.

Unaweza kutumia tangawizi, kitunguu saumu, ndimu pamoja na tandoori masala kuchemsha nyama mpaka iive na kulainika vizuri.

Wakati nyama inaiva, andaa viungo utakavyovitumia ikiwemo kitunguu maji, bilinganya, nyanya chungu, njegere, pilipili hoho, tui la nazi pamoja na pilipili.

Baada ya kumaliza maandalizi na nyama kuiva hatua inayofuata ni kuanza kuiunga nyama kwa viungo na nazi.

Bandika sufuria jikoni mimina mafuta kiasi, yakichemka weka vitunguu na ukoroge hadi vibadilike rangi.

Ongeza nyanya chungu, biringanya, karoti hoho, nyama pamoja na njegere zilizochemshwa, koroga vizuri ili viungo na nyama vichanganyike pamoja.

Dakika Moja au mbili zinatosha kabisa kuchanganya viungo na nyama, hatua inayofuata itakuwa kuongeza maji kiasi na kufunika mpaka viungo vikaribie kuiva.

Viungo vikaribia kuiva huo ndio wakati sahihi wa kuweka tui la nazi, kama unatumia nazi ya kukuna unaweza kutanguliza tui jepesi kwanza kisha ukamalizia na tui zito baadae, lakini kama unatumia nazi ya pakti utaweka yote katika hatua hii.

Tui likichemka vizuri na kutengeneza rojo nzito utaweka chumvi kiasi na hapo kitimoto nazi itakuwa tayari kwa kuliwa.

Msosi huu utanoga zadi ikiwa utasindikizwa na ndizi, chipsi, ugali au chapati.

Je una maujanja mapya ya mapishi ungependa kushea nasi, tupigie kupitia 0677088088 au tuandikie ujumbe kupitia jikopoint@nukta.co.tz.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV