Ni uzushi mtupu: Wakenya hawajaandamana kupinga zuio la kutotoka nje

May 23, 2020 3:27 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Picha ya maandamano yaliyotokea Mei 8 jijini Nairobi haina uhusiano na watu kupinga marufuku ya kutoka nje. 
  • Bali ni picha inayoelezea waandamanaji kupinga kutolewa katika nyumba walizokuwa wanakaa. 
  • Picha hiyo ni uzushi na haina ukweli wowote kuhusu Corona. 

Dar es Salaam. Kwa sasa katika mitandao ya kijamii ikiwemo Facebook na WhatsApp imesambaa picha ikionyesha watu wakiandamana nchini Kenya ikidaiwa kuwa wanapinga marufuku ya kutokutoka nje wakati huu wa janga la Corona. 

Picha hiyo imebeba ujumbe unaodai kuwa wananchi wa Kenya hawataki tena kukaa ndani na sasa wanashinikiza kuendelea na shughuli zao. 

Lakini kimsingi ujumbe uliowekwa katika picha hiyo hauna uhusiano wowote na watu kuandamana kupinga marufuku ya kutokutoka nje (lockdown) kwa sababu ya kujikinga na ugonjwa wa virusi vya Corona. 

Ukweli ni upi?

Timu ya Nukta Fakti imebaini kuwa tukio hilo ambalo liko kwenye picha hiyo limechukuliwa katika kipande cha video cha maandamano yaliyotokea nje kidogo ya  jijini Nairobi siku ya ijumaa Mei 8, 2020 na kuwekwa katika ukurasa wa Facebook wa The Star Kenya. 

Yalikuwa ni maandamano ya wakazi wa maeneo ya Korogocho and Kariobangi jijini humo baada ya kuondolewa katika nyumba zinazodaiwa kuwa ni za kampuni ya maji safi na taka jijini humo. 

Katika maandamano hayo, unaonekana moto unawaka katikati ya barabara za maeneo hayo huku mabomu ya machozi yakirushwa kuwatawanya waandamanaji. 


Zinazohusiana.


Tukio hilo halikutokea kwa sababu ya raia hao kupinga kutokuruhusiwa kutoka nje ili kujikinga na Corona. 

Video hiyo inayosambaa mtandaoni ikihusishwa na Corona ni uzushi na haina ukweli wowote kwa sababu ni ya tukio lingine kabisa. 

Hata hivyo, nchi hiyo imeyafunga baadhi ya maeneo ya nchi hiyo yenye maambukizi makubwa likiwemo jiji la Nairobi ili kuzuia kusambaa zaidi kwa virusi vya Corona. 

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV