Necta yatangaza matokeo ya darasa la nne, kidato cha pili ufaulu waongezeka kiduchu

January 10, 2026 3:17 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Ufaulu wa darasa la nne umeongezeka kwa asilimia 2.67 na kidato cha pili umeongezeka kwa asilimia 1.52.

Dar es Salaam. Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta) limetangaza matokeo ya upimaji wa kitaifa wa darasa la nne na kidato cha pili huku ufaulu ukiongezeka kiduchu.

Katibu Mtendaji wa baraza hilo, Dk Said Mohamed aliyekuwa akitangaza matokeo hayo leo Januari 10, 2026 amesema ufaulu wa darasa la nne umeongezeka kwa asilimia 2.67 na kidato cha pili umeongezeka kwa asilimia 1.52.

“Kwa upimaji wa darasa la nne, ufaulu umepanda kwa asilimia 2.67 ambapo wanafunzi 1,324, 970 sawa na asilimia 88.91 wamefaulu kwa kupata madaraja ya A,B,C na D….

….. Ufaulu wa kidato cha pili kwa mwaka 2025 umeimarika kwa ongezeko la asilimia 1.52 kutoka asilimia 85.41 na asilimia 85.31 ya mwaka 2023,” amefafanua Dk Mohamed.

Kwa mujibu wa Necta jumla ya wanafunzi 898,718 walisajiliwa kufanya upimaji wa kidato cha pili wakiwemo wasichana 497,891 na wavulana 400,827.

Kati ya hao, waliofanya mtihani huo uliofanyika Novemba, 2025 ni wanafunzi 811,575 sawa na asilimia 91.3 katika shule za sekondari 6,223 huku wanafunzi 77,689 sawa na asilimia 8.7 wakishindwa kufanya mitihani hiyo kwa sababu mbalimbali.

Kwa upande wa mtihani wa darasa la nne, Dk Mohamed amesema waliosajiliwa walikuwa 1,583,686 na waliofanya mitihani hiyo walikuwa 1,490,377 kutoka shule za msingi  20,508.

Upimaji huo wa darasa la nne kwa mwaka 2025 ulizingatia mitaala iliyoboreshwa yaani masomo tisa kwa darasa la nne ambapo matano yalikuwa ya lugha, mawili ya sanaa, mawili ya sayansi na hisabati.

Pamoja na kuingizwa kwa masomo hayo mapya Dk Mohamed amesema ufaulu wa masomo yote ni mzuri.

“Kwa ujumla, ufaulu katika masomo yote ni mzuri ufaulu wa somo la kiswahili ni asilimia 92.1, somo la kiingereza ni asilimia 72.71, somo la kifaransa wamefaulu kwa asilimia 95.73, kiarabu asilimia 80.45, kichina kwa asilimia 93.16, sayansi 87.93 na hisabati ni asilimia 81.44,” amesema Dk Mohamed.

Kwa upande wa kidato cha pili Necta imesema ilipima wanafunzi hao kwa mitaala miwili ambayo ni mtaala wa awali na mtaala ulioboreshwa kwa wanafunzi wa mkondo wa amali ambao umepimwa kwa mara ya kwanza.

Licha ya ingizo hilo jipya la mkondo wa upimaji Necta imesema ufaulu ni mzuri.

“Kwa kuzingatia ufaulu watahiniwa 240,469 wa kidato cha pili wamepata madaraja la kwanza mpaka la tatu, mwaka 2024 waliopata madaraja hayo walikuwa 239,707 sawa na asilimia 30.08,” amesema Dk Mohamed.

/
No matches found for this filter
22 May, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
23 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
23 May, 2026
No active movers today
Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MIKOA YA KIPOLISI ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI TANZANIA BARA 2025

MIKOA YA KIPOLISI ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI TANZANIA BARA 2025

Nukta TV

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

Nukta TV

MIKOA 5 ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI 2025 TANZANIA BARA

MIKOA 5 ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI 2025 TANZANIA BARA

Nukta TV