NBC ongezeni wigo wa kutoa huduma-Majaliwa

February 14, 2019 9:15 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Awataka kusogeza huduma zao karibu na wananchi ili kuwavutia kutunza fedha zao katika hali ya usalama badala ya kuzihifadhi majumbani.
  • NBC yasema mwaka wa fedha uliopita wamefanikiwa kutengeneza faida na kwamba wanatarajia kutoa tena gawio kwa Serikali.

Dar es Salaam. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameitaka Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) iongeze wigo wa kutoa huduma ili kuwafikia wananchi wengi na kuongeza usalama wa pesa zao. 

Majaliwa ametoa wito huo leo (Februari 14, 2019)  wakati akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Theobald Sabi ofisini kwake Magogoni, jijini Dar es Salaam, ambapo amesema wakati Serikali ikiendelea kuhamasisha wananchi waongeze nguvu katika sekta ya kilimo, taasisi za fedha hazina budi kusogeza huduma zao karibu na wananchi ili waweze kutunza fedha zao katika hali ya usalama badala ya kuzihifadhi majumbani.

 “Ninatoa wito kwenu mpanue wigo katika utoaji wa huduma zake hapa nchini ili kuwawezesha wananchi wengi zaidi kuhifadhi fedha zao katika eneo salama,” amesema Majaliwa.

Amesema benki  ya NBC imekuwa mstari wa mbele wa kuwawezesha wananchi kupitia mikopo kwa wajisiriamali wadogo ambayo inawawezesha kuongeza mitaji yao ya biashara mbalimbali.


Zinazohusiana: 


Kwa upande wake, Sabi ameishukuru Serikali kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya kufanya biashara na mwaka wa fedha uliopita wamefanikiwa kutengeneza faida na kwamba wanatarajia kutoa tena gawio. 

Hata hivyo, hakutaja ni kiasi gani cha gawio kitatolewa, kwa sababu anasubiri uamuzi wa Bodi.

Mei 2017, NBC ilitoa gawio la Sh1.7 bilioni kwa Serikali ambayo inamiliki asilimia 30 za hisa kwenye benki hiyo. 

Pia amemkabidhi Waziri Mkuu hundi yenye thamani ya Sh11.2 milioni ambazo amesema zitasaidia katika ujenzi wa kituo cha polisi wilayani Ruangwa.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV