MTN, Airtel yaripoti hasara mitandao ya kijamii ikifunguliwa Uganda

January 27, 2026 4:17 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni baada ya takriban siku 13 tangu kufungiwa kwa mitandao ya kijamii kupisha uchaguzi  mkuu.

Dar es Salaam. Serikali ya Uganda imefuta marufuku ya mitandao ya kijamii iliyokuwa imewekwa wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Januari 15, 2026, huku makampuni makubwa ya mtandao yakiripoti hasara ya Sh17.8 bilioni.

Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba katika taarifa yake iliyochapishwa jana Januari 26, 2026 katika mtandao wa X  amewashukuru wananchi wa Uganda kwa kushirikiana vyema katika kipindi chote cha marufuku hiyo.

“Tunafungua mitandao yote ya kijamii leo… Mungu awabariki wote,” amechapicha Muhoozi katika jukwaa la X.

Kufunguliwa kwa mitandao ya kijamii nchini humo kunakuja ikiwa ni takribani wiki mbili tangu kuanza kwa marufuku hiyo Januari 13, 2026, siku mbili kabla ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Januari 15, 2026.

Mbali na tukio hilo, kukosolewa vikali na wapinzani wa kisiasa na mashirika ya haki za kiraia, mamlaka za mawasiliano nchini humo zilisema hatua hiyo ililenga kulinda usalama wa Taifa, kuzuia habari zisizo sahihi na kuzuia vurugu za kisiasa

Ingawa huduma ya intaneti kwa ujumla ilianza kurejeshwa kidogo kidogo  kuanzia Januari 17 mwaka huu, bado wananchi walilazimika kutumia VPN ili kupata huduma za muhimu na kufanya miamala ya kidigitali hatua  ilioyopoteza mapato ya Sh 17.8 bilioni kwa kampuni kubwa za mawasiliano ikiwemo MTN na Airtel.

Kwa sasa, wananchi wa Uganda wanaweza kutumia mitandao ya kijamii bila VPN, jambo linaloashiria kurejea kwa hali ya kawaida ya shughuli za kidijitali. 

Hata hivyo, baadhi ya majukwaa kama Facebook bado yanaripotiwa kuwa na vizuizi vidogo au kutokuwa na ufikiaji bila VPN.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...

Enable Notifications OK No thanks