MTN, Airtel yaripoti hasara mitandao ya kijamii ikifunguliwa Uganda

January 27, 2026 4:17 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni baada ya takriban siku 13 tangu kufungiwa kwa mitandao ya kijamii kupisha uchaguzi  mkuu.

Dar es Salaam. Serikali ya Uganda imefuta marufuku ya mitandao ya kijamii iliyokuwa imewekwa wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Januari 15, 2026, huku makampuni makubwa ya mtandao yakiripoti hasara ya Sh17.8 bilioni.

Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba katika taarifa yake iliyochapishwa jana Januari 26, 2026 katika mtandao wa X  amewashukuru wananchi wa Uganda kwa kushirikiana vyema katika kipindi chote cha marufuku hiyo.

“Tunafungua mitandao yote ya kijamii leo… Mungu awabariki wote,” amechapicha Muhoozi katika jukwaa la X.

Kufunguliwa kwa mitandao ya kijamii nchini humo kunakuja ikiwa ni takribani wiki mbili tangu kuanza kwa marufuku hiyo Januari 13, 2026, siku mbili kabla ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Januari 15, 2026.

Mbali na tukio hilo, kukosolewa vikali na wapinzani wa kisiasa na mashirika ya haki za kiraia, mamlaka za mawasiliano nchini humo zilisema hatua hiyo ililenga kulinda usalama wa Taifa, kuzuia habari zisizo sahihi na kuzuia vurugu za kisiasa

Ingawa huduma ya intaneti kwa ujumla ilianza kurejeshwa kidogo kidogo  kuanzia Januari 17 mwaka huu, bado wananchi walilazimika kutumia VPN ili kupata huduma za muhimu na kufanya miamala ya kidigitali hatua  ilioyopoteza mapato ya Sh 17.8 bilioni kwa kampuni kubwa za mawasiliano ikiwemo MTN na Airtel.

Kwa sasa, wananchi wa Uganda wanaweza kutumia mitandao ya kijamii bila VPN, jambo linaloashiria kurejea kwa hali ya kawaida ya shughuli za kidijitali. 

Hata hivyo, baadhi ya majukwaa kama Facebook bado yanaripotiwa kuwa na vizuizi vidogo au kutokuwa na ufikiaji bila VPN.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
7 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
7 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV