Mtindo huu wa maisha unaiweka afya yako hatarini

November 11, 2021 11:14 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni matumizi ya pombe, uvutaji wa sigara, matumizi ya vyakula vyenye mafuta na kutokufanya mazoezi.
  • Husababisha magonjwa ya kisukari, moyo, saratani, figo na shinikizo la damu. 

Dar es Salaam. Watanzania ambao wanaendekeza mfumo wa maisha usiofaa ukiwemo unywaji pombe uliopitiliza wametakiwa kuachana na tabia hizo kwa sababu wanachangia kuongezeka kwa magonjwa yasiyoambukiza na hivyo kupunguza nguvukazi ya Taifa.

Mkurugenzi Msaidizi wa Magonjwa yasiyoambukiza  Dk James Kiholongwe akizungumza wakati akitoa elimu kwenye wiki ya kudhibiti magonjwa yasiyokuwa yakuambukiza jijini Dodoma  amesema kuwa kuna kila sababu ya jamii kujizuia kuishi maisha yanayoweza kuathiri afya.

Dkt. Kiholongwe amesema kuwa, watu wengi ambao wamekithiri katika matumizi ya pombe, uvutaji wa sigara, matumizi ya vyakula vyenye mafuta na kutokufanya mazoezi wamejikuta kwenye wimbi la kupata magonjwa yasiyokuwa ya kuambukiza na kulibebesha Taifa mzigo mzito.

Ameyataja baadhi ya magonjwa hayo kuwa ni kisukari, ugonjwa wa moyo, saratani, figo na shinikizo la damu ambayo vichocheo vikubwa ni kuishi mtindo usiofaa wa maisha usioendana na ulaji wa vyakula na vinywaji vinavyotakiwa.

Aidha, Dk Kiholongwe ameitaka jamii kujenga utaratibu wa kufanya mazoezi na kupima afya mara kwa mara Ili kujua mwenendo wa afya kwani itasaidia kujiepusha na magonjwa hayo.

                         

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV