Moto, afya, vyombo vya moto vinavyotawala soko la bima Tanzania

March 1, 2019 8:51 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Robo tatu ya tozo za bima nchini zililipwa na wateja mbalimbali nchini kwa ajili ya kununua huduma za bima za majanga ya moto, afya na vyombo vya moto kati ya Januari hadi Septemba 2018, Ripoti ya Mamlaka ya Bima (Tira) inaeleza.

Ripoti ya soko kwa sekta ya bima ya Januari hadi Septemba 2018 ya Tira inaeleza kuwa jumla ya tozo za bima (General insurance premiums) za Sh449.3 bilioni zililipwa katika kipindi hicho ikiwa ni ongezeko la asilimia 4.2 kutoka Sh431.3 bilioni zilizorekodiwa muda kama huo mwaka 2017.

Enable Notifications OK No thanks