Mkaa, mbogamboga vyachangia kupandisha mfumuko wa bei Tanzania

August 10, 2020 11:28 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Mfumuko huo wa bei umepanda hadi asilimia 3.3 mwaka ulioishia Julai 2020 kutoka asilimia 3.2 mwaka ulioishia Juni mwaka huu.

Dar es Salaam. Mfumuko wa bei kwa mwaka ulioshia Julai 2020 umeongezeka kidogo kufikia asilimia 3.3 kutoka asilimia 3.2 iliyorekodiwa mwaka ulioishia Juni mwaka huu ukichangiwa zaidi na kuongezeka kwa bidhaa za chakula na zisizo za chakula kama mkaa, unga wa mahindi, gesi ya kupikia na mbogamboga.

Mfumuko wa bei hupima kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma zinazotumiwa na kaya binafsi nchini.

Taarifa ya mfumuko wa bei iliyotolewa Agosti 10 2020 na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) inaeleza kuwa baadhi ya bidhaa za chakula zilizochangia kuongezeka kwa mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia Julai 2020 ni unga wa mahindi uliopanda kwa asilimia 7.9, mtama (asilimia 4.8), matunda (asilimia 4) na mbogamboga kwa 9.6.

“Kwa upande mwingine baadhi ya bidhaa zisizo kuwa za vyakula zilizoongezeka bei kwa mwezi Julai 2020 ikilinganishwa na Julai 2019 ni pamoja na mavazi yaliyopanda kwa asilimia 2.8, gesi ya kupikia kwa asilimia 5.9, samani (asilimia 2.7), gharama za ujenzi na ukarabati nyumba (asilimia 6.2) na mkaa kwa asilimia 11.6,” imesema sehemu ya taarifa hiyo ya NBS.


Zinazohusiana: 


Mfumuko huo wa bei umeongezeka kidogo baada ya kudumu katika kiwango cha asilimia 3.2 kwa miezi miwili mfululizo ya miaka inayoishia Mei na Juni mwaka huu.

Hata hivyo, kasi ya mfumuko wa bei za vyakula na vinywaji baridi kwa Julai 2020 umeendelea kubaki katika asilimia 3.8 kama ilivyokuwa Juni 2020.

Kiwango cha mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia Julai 2020 nchini Tanzania ni cha chini ikilinganishwa na viwango vya nchi jirani za Afrika Mashariki za Kenya na Uganda.

Mfumuko wa bei kwa Julai mwaka huu nchini Kenya ulipungua na kufikia asilimia 4.36 kutoka asilimia 4.59 mwaka ulioishia Juni.

Huko Uganda, mfumuko wa bei kwa kipindi hicho uliongezeka hadi asilimia 4.7 kutoka asilimia 4.1 mwaka ulioishia Juni 2020, kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyotolewa na Mtakwimu Mkuu, Dk Albina Chuwa.

Mbogamboga ni moja ya bidhaa za chakula zinazotumika na kaya nyingi Tanzania. Bidhaa hizo ziliongezeka bei Julai 2020 ikilinganishwa na iivyokuwa Julai mwaka jana. Picha|Emanuel Feruzi/K15.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV