Mauzo ya madini nje ya nchi yaongezeka Tanzania

Sekta ya madini nchini imeendelea kuimarika na kuongeza mchango wake katika uchumi wa Taifa, huku mapato ya fedha za kigeni yatokanayo na mauzo ya madini nje ya nchi yakiongezeka kwa asilimia 31.1 katika mwaka wa fedha 2025/26.
Kwa mujibu wa takwimu zilizowasilishwa na Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, wakati akiwasilisha hotuba ya bajeti ya wizara hiyo Aprili 27, 2026 mapato hayo yaliongezeka kutoka Dola za Marekani milioni 4,119 mwaka 2024/25 hadi Dola milioni 5,401.9 mwaka 2025/26.