Mambo ya kufanya kulinda afya ya macho yako

April 19, 2021 9:19 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni pamoja na kuepuka kutumia dawa bila maelekezo ya daktari.
  • Unashauriwa kupima macho mara kwa mara. 

Dar es Salaam. Kadiri umri unavyozidi kusogea uzeeni, viungo vya mwili taratibu huanza kupungukiwa uwezo wake wa kufanya kazi. Kuanzia miguu, mgongo na vivyo hivyo kwa macho. 

Hata hivyo, kwa namna moja ama nyingine, tabia zetu za kila siku zinaweza kuharakisha au kupunguza kasi ya kupungua kwa uwezo wa kuona.

Kwa mujibu wa Daktari na Mtafiti kutoka Taasisi ya Afya ya Jamii (KCMUco), Dk Julieth Sebba, yapo mazoezi au tabia nzuri zinazoweza kuifanya afya ya macho yako kuwa nzuri kadri umri wako unavyozidi kusogea.

Epuka matumizi ya sigara, dhibiti magonjwa kama kisukari na presha ya damu na epuka matumizi ya dawa za macho bila ushauri wa mtaalamu wa afya.

Kufahamu zaidi, tazama video hii:

                         

Enable Notifications OK No thanks