Majaliwa awakaribisha wawekezaji kutoka Vietnam kujenga viwanda

July 3, 2019 12:19 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Balozi wa Vietnam nchini Tanzania, Nguyen  Doanh, ofisini kwa Waziri Mkuu, Magogoni jijini Dar es salaam, Julai 3, 2019. Picha|Ofisi ya Waziri Mkuu.


  • Amesema viwanda hivyo vitakuwa vinatumia malighafi za kilimo ili kuwafaidisha wakulima wa Tanzania.
  • Wafanyabiashara wa Vietnam nao wakaribishwa kununua korosho na kahawa ya Tanzania. 
  • Naibu Waziri Mkuu wa Vietnam, Trinh Dinh Dung kuingia Tanzania wiki ijayo. 

Dar es Salaam. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amewakaribisha wawekezaji kutoka nchi ya Vietnam waje Tanzania kuwekeza katika sekta ya viwanda vinavyotumia malighafi za kilimo ili wakulima wapate soko la uhakika la mazao yao.

Amesema Serikali imeanzisha Wizara ya Uwekezaji iliyo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa ajili ya kuifanya Tanzania kuwa ni mahali bora na salama kwa wawekezaji na wafanyabiashara.

Majaliwa ametoa wito huo leo (Julai 3, 2019) wakati akizungumza na Balozi wa Vitemam nchini Tanzania, Nguyen Doanh ofisini kwake, Magogoni jijini Dar Es salaam. 

“Serikali imeendelea kuondoa  vikwazo vya  kuanzisha na kuendesha  biashara  kwa kupitia upya   sheria, kanuni na taratibu za biashara  na kuzifuta zile  ambazo zimethibitika  kuwa zinayafanya mazingira ya biashara na uwekezaji nchini kuwa magumu,” amesema Majaliwa. 

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu, Vietnam imepiga hatua kubwa katika ujenzi na uendeshaji wa viwanda vya nguo, Tanzania ingefurahi kuona viwanda vya aina hiyo vinajengwa hapa nchini na wawekezaji wa nchi hiyo.

Amesema kuwa ununuzi wa mazao ya kilimo kama vile pamba, korosho, kahawa na tumbaku ni fursa nyingine ya kibiashara ambayo wafanyabiashara wa Vietnam wanakaribishwa kuichangamkia ili wanufaike na mazao hayo.


Zinazohusiana:


Tanzania na Vietnum zimekuwa na ushirikiano wa muda mrefu katika nyanja mbalimbali ikiwemo sekta ya mawasiliano ambapo nchi hiyo ina kampuni ya simu za mkononi ya Halotel inayoendesha shughuli zake nchini. 

Balozi Doanh ametumia fursa hiyo kumweleza Waziri Mkuu juu wa ujio wa Naibu Waziri Mkuu wa Vietnam, Trinh Dinh Dung anayetarajiwa kufanya ziara yake ya kikazi nchini kuanzia Julai 9 hadi 11 mwaka huu. 

Amesema Dung huyo anatarajiwa kuambatana na wafanyabiashara wasiopungua 20 kutoka kampuni kubwa za nchini Vietnam.

Nchi za Vietnam na Tanzania zilianzisha uhusiano wa kidiplomasia mwaka 1965. Mwaka 1984, Vietnam ilifunga ofisi ya Ubalozi  wake hapa nchini kwa muda na kuufungua upya mwaka 2003.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV