Mabango ya kielektroniki KIA kukuza utalii kaskazini

April 29, 2019 5:10 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akifurahia jambo na watalii kutoka Israeli mara baada ya kuwaaga katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA). Picha|Ofisi ya Waziri Mkuu.


  • Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameiagiza Bodi ya Kampuni ya Uendeshaji wa Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro (Kadco) kuweka mabango ya kielektroniki yanayoonyesha vivutio vya utalii katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Dar es Salaam. Huenda utalii katika mikoa ya kaskazini mwa Tanzania ukapata msukumo wa aina yake, baada ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuiagiza Bodi ya Kampuni ya Uendeshaji wa Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro (Kadco) kuweka mabango ya kielektroniki yanayoonyesha vivutio vya utalii katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Majaliwa aliyekua akikagua miundombinu ya uwanja wa ndege wa KIA mara baada ya kuwaaga watalii 274 kutoka Israeli waliowawakilisha wenzao 1,000 kuondoka nchini juzi (Aprili 27, 2019) kurejea kwao, amesema Kadco washirikiane na Wizara ya Maliasili na Utalii kuweka utaratibu mzuri wa kutangaza vivutio katika uwanja huo ili kuongeza mapato kwa Serikali.

“Kadco na Wizara ya Maliasili na Utalii, shirikianeni kuweka utaratibu wa kutangaza vivutio vyetu vya utalii hasa wanyama kwenye viwanja vyote vya ndege. Tunazo mbuga, milima, fukwe za bahari na ngoma za makabila mbalimbali, wekeni mabango yanayobadilisha picha,” amesema Majaliwa. 


Zinazohusiana: 


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu, uongozi wa kampuni hiyo umetakiwa uangalie namna ya kutumia kuta zake kwa kuweka picha zinazoonyesha makabila na shughuli za utamaduni wa Tanzania ili kuwawezesha wageni wanaotumia uwanja huo kufahamu kwa undani fursa za utalii zilizopo nchini.

“Nimezunguka humu ndani, kuta zote ni nyeupe tu, tumieni fursa hiyo kutangaza tamaduni zetu na vivutio tulivyonavyo,” amesema Majaliwa wakati akimpa maelekezo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kadco, Mhandisi Christopher Mukoma. 

Akiwa uwanjani hapo, Waziri Mkuu amekagua eneo la mapokezi, sehemu ya abiria wanaoondoka na wanaowasili, sehemu ya uhamiaji, mashine za kukagua mizigo ya wanaoondoka na wanaowasili, sehemu za kutolea huduma na maduka.

Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji wa KIA, Filbert Ndege ameagizwa awasiliane na makao makuu ya Idara ya Uhamiaji ili waangalie uwezekano wa kuongeza madirisha ya kutolea huduma za uhamiaji (counters) ili huduma hiyo itolewe kwa kasi zaidi hasa msimu ambao watalii wengi huingia nchini.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
21 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
21 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
21 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Nukta TV

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Nukta TV

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

Nukta TV