Lindi, Mtwara zinavyochuana kidato cha sita

July 13, 2019 1:03 pm · Daniel
Share
Tweet
Copy Link
  • Mikoa ya Lindi na Mtwara toka mwaka 2017 hazijawi kushuka nafasi ya tatu.
  • Mkoa wa Lindi mwaka huu 2019 umefaulisha wanafunzi wote kwa asilimia 100 kama ilivyofanya Mtwara mwaka 2018.

Dar es Salaam.Katika matokeo ya kidato cha sita yaliyotangazwa na Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta) wiki hii, yameuweka mkoa wa Lindi katika nafasi ya kwanza kitaifa kwa mpangilio wa ufaulu wa mikoa 29 iliyoshiriki mtihani huo. 

Lindi imeshika nafasi ya kwanza baada ya kupanda kutoka nafasi ya pili iliyoshikilia mwaka 2018  na kuushusha mkoa jirani wa Mtwara kwa nafasi mbili kutoka namba mmoja mwaka 2018 hadi nafasi ya tatu mwaka huu. 

Mafanikio iliyopata Lindi, siyo tu ni somo kwa mikoa mingine bali kwa wadau wa elimu kuwekeza zaidi katika elimu ili kuhakikisha wanafunzi wanapata maarifa sahihi kuwawezesha kujibu mtihani. 

Uchambuzi uliofanywa na www.nukta.co.tz wa mpangilio wa mikoa kwa ubora wa ufaulu katika mtihani wa kidato cha sita uliotolewa na Necta mwaka 2019 unaonyesha kuwa siyo tu Lindi imeongaza kitaifa bali  wanafunzi wake wote  wamefaulu kwa asilimia 100. 

Wanafunzi wote 953 waliofanya mtihani huo kutoka katika shule tisa za mkoa huo  wamefaulu kwa kupata kati ya daraja la I hadi IV na hakuna mwanafunzi hata mmoja aliyepata daraja sifuri. 

Hali imekuwa ni tofauti na  mwaka uliopita (2018) ambapo mkoa huo ulishika nafasi ya pili kitaifa huku ukifaulisha kwa asilimia 99.59  ambapo wanafunzi 733 kutoka shule nane walifaulu kwa kupata kati ya  daraja la I hadi IV.Wanafunzi watatu tu walipata daraja sifuri kati yao wawili walitoka Shule ya Sekondari  Mahiwa  na mmoja alitoka Seminari ya Namupa.

Shule ya Sekondari Lindi iliyopo mkoa wa Lindi ambayo nayo imefanya vizuri katika mkoa huo. Picha|Mtandao.

Kwa mujibu wa viwango vya ufaulu vya Necta wanafunzi wanaopata daraja la I hadi la IV wanahesabika wamefaulu na wana sifa ya kupata cheti na kuendelea na masomo ya elimu ya juu.

Katika matokeo hayo yalitangazwa alhamisi (11 julai 2019) yanaonyesha kuwa zaidi ya nusu ya wanafunzi wamepata daraja la pili, sawa na asilimia 57 ya wanafunzi wote waliofanya mtihani huo mkoani humo.

Kwa upande wa daraja IV ni wanafunzi  sita tu walifaulu katika daraja hilo sawa na asilimi 0.6 huku daraja la III wakiwa wanafunzi 175.

Wakati Mkoa wa Mtwara ukipigwa kikumbo na Lindi, nao bado uko katika nafasi nzuri  ambapo mwaka huu  umeshika nafasi ya tatu kitaifa nyuma ya Mkoa wa Singida uliopanda kutoka nafasi ya saba mwaka 2018. 

Huku pia asilimia ya wanafunzi waliopata daraja II ikishuka hadi kufikia asilimia 48.3 mwaka 2019 kutoka asilimia 56 ya wanafunzi wote waliofanya mtihani huo. Lakini wanafunzi waliopata daraja IV mwaka 2019 wameongezeka kutoka wanafunzi 11 mwaka 2018 hadi 18 mwaka huu ambapo waliopata sifuri ni sita. 


Zinazohusiana: 


Matokeo hayo ni ya kubahatisha?

Historia ya ufaulu wa elimu katika  ya mikoa hiyo ya Lindi na Mtwara siyo ya kubahatisha ni  ya muda kidogo na nyakati zote wanafunzi wake wamekuwa wakifaulu.

Takwimu za Necta zinaonyesha kuwa kwa miaka mitatu iliyopita, mikoa hiyo imekuwa ikishikilia nafasi tatu za juu katika ubora wa ufaulu kwa mikoa. 

Mwaka 2017 mkoa wa Lindi ulishika nafasi ya pili sawa sawa na mwaka jana kabla ya kupanda hadi katika nafasi ya kwanza mwaka huu. 

Kwa upande wa Mtwara, mwaka 2017 ulishika nafasi ya tatu kitaifa na mwaka uliofuatia ikawa ya kwanza kabla ya kushuka hadi nafasi ya tatu mwaka huu. 

Matokeo hayo yameibua shangwe kwa viongozi wa mkoa huo, akiwemo Mbunge wa Mtama mkoani Lindi, Nape Nnauye ambaye katika ukurasa wake wa Twitter ameandika,

“Mwenyezi Mungu hakunyimi kila kitu! Mkoa wa Lindi umekuwa wa Kwanza kitaifa matokeo ya kidato cha sita. Na kati ya wanafunzi kumi bora kitaifa mmoja katoka jimbo la Mtama, Shule ya Sekondari Nyangao!.”

Siku chache kabla ya kufanyika kwa mtihani wa kidato cha sita mwaka huu, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara aliambia www.nukta.co.tz kuwa ufaulu mzuri katika mkoa wake unachangiwa na ushirikiano baina ya walimu, wanafunzi na viongozi wa mkoa huo kufuatilia masomo darasani.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
21 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
21 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
21 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Nukta TV

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Nukta TV

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

Nukta TV