Kifo cha Magufuli chaahirisha sherehe za Muungano wa Tanzania

April 26, 2021 7:05 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Serikali imesema haijafanya sherehe za Muungano mwaka huu kutokana na kifo cha Hayati John Magufuli.
  • Muungano wa mwaka huu unaadhimishwa kwa kongamano maalum jijini Dodoma.
  • Fedha za sherehe hizo kugawanywa Tanzania Bara na Zanzibar. 

Dar es Salaam. Makamu wa Rais Dk Philip Mpango amesema Serikali iliamua kutokufanya sherehe za Muungano wa Tanzania mwaka huu kutokana na tukio la hivi karibuni la kifo cha Hayati Rais John Magufuli. 

Hayati Dk Magufuli alifariki dunia Machi 17 mwaka huu kwa maradhi ya moyo ambapo nafasi yake imechukuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Badala yake sherehe hizo za kuadhimisha miaka 57 ya muungano zinaadhimishwa kwa kongamano maalum linalowakutanisha wasomi na Watanzania katika ukumbi wa Chimwaga jijini Dodoma. 

Dk Mpango aliyekuwa akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo leo Aprili 26, 2021 amesema imekuwa ni utamaduni wetu kuadhimisha sherehe za muungano kitaifa kwa gwaride maalum na burudani katika kiwanja mahususi lakini mwaka huu ni tofauti.

“Lakini kwa mwaka huu kutokana na tukio la hivi karibuni ambapo nchi yetu iliondokewa na mmoja wa mashujaa wetu Hayati John Magufuli aliyekua kiongozi mkuu wa Taifa letu, tuliamua badala ya sherehe tuadhimishe kwa kongamano hili,” amesema Dk Mpango.


Soma zaidi: 


Amesema fedha zilizotengwa kwa sherehe hizo zitagawanywa pande zote mbili za muungano yaani Tanzania Bara na Zanzibar na kila mmoja ataamua matumizi yake.

Aidha, Makamu wa Rais amewataka Watanzania kuendelea kuuenzi muungano kwa kudumisha umoja wa kitaifa, ulinzi na usalama. 

Amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia imelifanya suala la muungano kama moja ya vipaumbele vyake na itaulinda na kuuendeleza kwa vizazi vijavyo.

“Watakaojaribu kuchezea muungano, hapo mimi sitakuwa mpole,” amesema Dk Mpango katika hutuba yake.

Muungano wa Tanzania ni matokeo ya kuungana kwa nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar Aprili 26, 1964. Waliosisi ni Rais wa kwanza wa Tanzania Hayati Julius Nyerere na Sheikh Abeid Karume, aliyekuwa Rais wa kwanza wa Zanzibar.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
16 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
17 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
17 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Nukta TV

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Nukta TV

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Nukta TV