Kamati yabaini matatizo maabara ya kupima corona Tanzania

May 23, 2020 3:22 pm · Nuzulack Dausen
Share
Tweet
Copy Link
  •  Imebaini mashine mojawapo ya kupima corona ilikuwa na matatizo kwa takriban mieizi miwili.
  • Serikali yaanza kupima corona katika maabara mpya.

Dar es Salaam. Serikali imesema kamati iliyoundwa kuchunguza maabara ya taifa ya jamii kuhusu mwenendo wa upimaji virusi vya corona imethibitisha mashaka aliyokuwa nayo Rais John Magufuli baada ya kubaini kuwa moja ya mashine za kupimia virusi hivyo ilikuwa na hitilafu kwa takriban miezi miwili.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto amewaambia wanahabari jijini Dar es Salaam kuwa kamati hiyo imebaini mapungufu katika kadhaa katika shughuli hiyo ya upimaji wa ugonjwa wa virusi vya Corona (COVID-19).

Mapema mwezi huu waziri huyo aliunda kamati ya wataalamu 10 kuchunguza kwa kina mwenendo wa utendaji wa maabara ya Taifa ya jamii katika upimaji wa COVID-19 baada ya Rais Magufuli kuonyesha mashaka kutokana na vipimo hivyo kubaini baadhi ya vitu visivyo binadamu kama mbuzi na papai kuwa na corona.

“Mojawapo ya mashine za kupima sampuli za COVID-19 ilikuwa na hitilafu kwa takriban miezi miwili bila ya uongozi wa maabara kuchukua hatua za kuifanyia matengenezo,” amesema Ummy Jumamosi (Mei 23, 2020).

Ummy amesema kamati hiyo imebaini kuwepo kwa mapungufu katika mfumo wa kimuundo, kiutendaji na uendeshaji wa kitaaluma katika upimaji wa vipimo, uhakiki wa ubora wa majibu.


Soma zaidi: 


Kamati hiyo, iliyokuwa ikiongozwa na Profesa Eligius Lyamuya wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba Muhimbili (Muhas), imebaini pia udhaifu katika uhifadhi wa vipimo vya COVID-19.

“Aidha, imebainika uwepo kwa upungufu wa wataalamu wenye sifa mafunzo ya biotechnology (Bioteknolojia) and ‘molecular biology’ katika sekta ya afya ikiwemo katika maabara kuu ya taifa ya afya iliyopo NIMR,” amesema waziri huyo.

Katika kuboresha shughuli za upimaji, Ummy amesema hivi sasa upimaji wa sampuli zote za COVID-19 unahamishiwa katika maabara mpya ya Taifa ya jamii iliyopo Mabibo jijini Dar es Salaam na kutoka katika maabara ya zamani iliyopo ofisi za Taasisi ya Taifa ya utafiti wa magonjwa ya binadamu (NIMR).

Ummy amesema wameshaandaa wataalam wenye sifa na vigezo kwa ajili ya maabara hiyo mpya na kwamba wameanza kurekebisha mfumo wa utawala, utendaji na kitaaluma ndani ya maabara ya Taifa. 

Kituo cha Kudhibiti Magonjwa cha Afrika (AfrikaCDC) kimebainisha kuwa hadi Mei 23 Tanzania ilikuwa imerekodi wagonjwa 509 wa corona. Kati ya hao, 167 wameshapona ugonjwa huo huku 21 wakipoteza maisha.

Tanzania haijatangaza wagonjwa wapya tangu Aprili 29 mwaka huu. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV