Kamanda Muliro aondoka Mwanza na tukio lisilosahaulika

June 2, 2021 5:57 am · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni Kamanda Jumanne Muliro aliyehamishiwa Mkoa wa Dar es Salaam.
  • Anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Camilius Wambura aliyeteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI).
  • Amesema hatasahau tukio la kizushi la kukamatwa kwa vichwa 20 vya watoto katika kituo cha polisi Nyakato.

Mwanza. Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jumanne Muliro aliyehamishiwa Mkoa wa Dar es Salaam amesema hatasahau tukio la kizushi la kukamatwa kwa vichwa 20 vya watoto katika kituo cha polisi Nyakato mkoani humo, jambo lililoibua taharuki kubwa kwenye jamii.

Kamanda Muliro anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Camilius Wambura ambaye amepandishwa cheo na kuwa Kamishna wa Polisi na kuteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI).

Amesema tukio hilo lilitokea Februari  20, 2019 ambapo waandishi wa habari walilipoti taarifa hiyo bila kuwa na uhakika wa tukio lenyewe, jambo lililomuweka katika wakati mgumu kiuetendaji.  

“Ni nitukio ambalo lilitengeneza taharuki kwa wananchi na hata vyombo vya dola vilitahamaki, lakini tunashukru uongozi wa waandishi wa habari mkoa wa Mwanza tulikaa pamoja kuhakikisha suala hilo linatatuliwa,”amesema Kamanda Muliro.

Amesema tukio lilikuwa siyo la kweli na kulikuwa hakuna taarifa za kutosha.  


Soma zaidi: 


Hata hivyo, Kamanda huyo amewashukuru waandishi wa habari kwa kuwa sehemu ya kazi yake na kwamba wamemsaidia katika kuibua matukio mengi na kumpatia taarifa kwa ajili ya ufuatiliaji mkoani humo.

“Waandishi wa habari kwangu wamekuwa kama mbwa wanaobweka pale wanapoona kuna hatari yaani “watch dog”, wamenisaidia sana  katika mfumo wa utendaji kazi na pia wamechangia katika kuufanya Mkoa wa Mwanza kuwa tulivu,” amesema. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Nukta TV

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Nukta TV

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Nukta TV