Jinsi ya kupika wali wa zabibu

August 14, 2023 1:26 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Chakula hiki ni mbadala kwa wasiopenda pilau lenye viungo vingi.
  • Unachohitaji ni mchele, zabibu,mafuta na chumvi.
  • Unaweza kuongeza viungo vingine kama njegere na kitunguu swaumu.

Waliosema ‘mchele mmoja mapishi mengi’ hawakukosea, siku hizi kuna aina mbalimbali za mapishi yanayoweza kubadili ratiba yako ya mlo uliyoizoea kila siku.

Wengi wetu tumezoea kula zabibu kama miongoni mwa matunda yenye ladha tamu na virutubisho mbalimbali, lakini umeshawahi kula wali wa zabibu?.

Wali huu ni mtamu na unaweza kutumika pia kama mbadala kwa watu wasiopenda pilau la zabibu lenye viungo vingi.

Si hayo tu, zabibu inayotumika kwenye chakula hiki imesheheni vitamini A,B, C, na K inayoweza kuimarisha afya ya macho na mifupa.

Kama hujawahi kula wali wa zabibu upo mahali sahihi, twende pamoja mpaka mwisho wa makala hii tunapojifunza jinsi ya kupika wali huu.

Maandalizi

Mapishi ya wali wa zabibu yanaanza kwa kuchambua mchele na kuandaa zabibu kavu ambazo ndizo hutumika katika aina hii ya mapishi.

Zabibu kavu zinazotumika katika pishi hili  zinapatikana katika ‘super markets’, kwenye maduka ya nafaka na sokoni. 

Kama utapendelea kuweka njegere na vitunguu swaumu huu ndio wakati sahihi wa kuviandaa pia ili kutumia muda mchache wakati wa kupika.

Baada ya kuandaa mahitaji yote washa jiko na uchemshe maji utakayoyatumia kupika wali, yakichemka yaweke pembeni na ubandike sufuria nyingine.

Sufuria ikipata moto weka mafuta ya kupikia kiasi kisha uweke kitunguu swaumu ulichokiponda pamoja na kitunguu maji kama utapendelea kisha ukoroge kwa dakika moja.

Ukiona vitunguu vyako vimeiva na kutoa manukato mimina mchele, njegere, chumvi kiasi na kijiko kimoja cha manjano yatakayofanya wali wako uwe na rangi ya kuvutia kisha koroga na ufunike uive.

Kwa wanaotumia nishati safi ya kupikia kama gesi au jiko la umeme hakuna ulazima wa kupalia makaa, funika wali wako vizuri na mfuniko usiopitisha hewa, punguza moto na uache uive taratibu.

Kama unatumia ‘rice cooker’ au ‘pressure cooker’ basi vuta kiti ukae maana ukifunika tu na kuseti kiwango cha moto wali wako utaiva wenyewe kwa haraka bila kuhitaji uangalizi wa mara kwa mara.

Wali wako ukikaribia kuiva mimina zabibu kiasi chako kisha ufunike wali uive vizuri na ladha ya zabibu iiingie kwenye chakula.

Baada ya muda tazama chakula chako kama kiveiva, geuza ili zabibu zisambae katika chakula chote kisha msosi wako utakuwa tayari kwa kuliwa.

Unaweza ukala chakula hiki na maini, nyama, samaki au mboga yoyote ya mchuzi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
12 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
12 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV