Jinsi ya kukabiliana na ugonjwa wa “Tonsillitis”

February 22, 2021 10:59 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Ugonjwa huo husababishwa na tishu za tonsils kuzidiwa na bakteria au virusi.
  • Hali hiyo hutokana nakula chakula kilicho na vimelea hivyo au kushika mdomo bila kunawa.
  • Kuepukana na tonsillitis, epuka unywaji wa maji ya baridi sana na kula chakula bila kunawa.

Dar es Salaam. “Tonsils” ni tishu zilizopo katika kila upande wa nyuma wa koo lako. Kwa mujibu wa tovuti ya afya (webmd) tishu hizo hunasa vijidudu ambavyo winaweza kuingia katika mfumo wa hewa na kusababisha maambukizi.

Hata hivyo, pale tishu hizo zinapoelemewa na vijidudu hivyo, huvimba na kumsababishia mtu maumivu makali sehemu ya koo  ikiambatanana shida zingine kiafya.

Hali hiyo wengi huuita “Matonsezi” lakini kitaalamu ni “Tonsilitis” na  ni tatizo ambalo huwapatia maumivu wakati wa kumeza kitu na hata wakati wa kukohoa au kupiga chafya. 

Mtu ambaye amepata tonsillitis hukabiliana na dalili kadhaa ikiwemo homa, kichwa kuuma, shida ya kumeza, maumivu  ya masikio na kinywa kutoa harufu mbaya.

Viashiria vingine vya ugonjwa huu kwa mujibu wa webmd ni kuwa na sauti kavu, kupata vidonda kooni, kukosa hamu ya chakula na kuvimba sehemu ya koo au taya. 

Kwa watoto, baadhi hutapika, kupata maumivu ya tumbo na kukataa chakula.

Ugonjwa huo husababishwa na kula chakula kilicho na vimelea au kushika mdomo ukiwa na mikono michafu na kwa watoto, hili hutokea kwa kunyonya vidole baada ya kuwa wamecheza eneo ambalo sio safi.

Unawezaje kukabiliana na ugonjwa wa Tonsilitis? Tazama video hii kujifunza zaidi

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW