Jinsi ya kuchoma mishkaki kwenye jiko la umeme

March 15, 2022 5:42 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Unatakiwa kuwa na jiko la kuchomea nyama linalotumia umeme.
  • Jiko hilo linaweza kuchoma vyakula vyote na siyo nyama tuu.
  • Gharama yake ni kuanzia Sh70,000 hadi Sh100,000.

Kati ya sababu ambazo watu huzitumia kuendela kutumia mkaa ni mapishi ya nyama ya kuchoma, ni kutokufahamu njia nyingine za kuchoma nyama kwa kutumia nishati mbadala.

Utasikia mtu akisema “unachomaje mishkaki kwenye jiko la gesi?” Jibu linaweza lisiwe rahisi kulipata kama hujui nishati mbalimbali za kupikia.

Jiko Point hatuongelei nadharia, tunaongelea mambo ambayo yanashikika na baadhi ya watu tayari wanayatumia.

Katika pita pita zangu mjini Instagram hivi karibuni, nilikutana na ukurasa wa bidhaa za jikoni na mdau huyo (vadeeonline) alikuwa akionyesha namna jiko la kuchoma mishikaki linavyofanya kazi.

Kati ya vitu vilivyonivutia zaidi ni kuwa, unachohitaji kutumia jiko hilo, ni umeme tu. Siyo mkaa wala kuni, ni umeme.

Kwenye jiko hilo unaweza kuchoma nyama pamoja na vyakula vingine kama mahindi. Picha| Daraz.

Linafanyaje kazi?

Unachotakiwa ni kuandaa mishikaki yako kwa kuikata na kuiweka kwenye vijiti vyake. Katika uchomaji wa mishikaki, inashauriwa kuunga nyama na viungo vya kulainisha nyama kama tangawizi na kitunguu swaumu.

Baada ya kuandaa mishkaki, andaa jiko lako la kuchomea vyakula kwa ajili ya kuchoma nyama. Maandalizi ya jiko hilo ni pamoja na kuweka trei ya kunasia mafuta.

Washa jiko lako na acha moto ukolee. Utajua kuwa moto umekolea kwa kuona koili za jiko lako zimeanza kuwa rangi ya machungwa. Bada ya hapo anza kuchoma mishkaki uliyoiandaa.

Hakikisha unasafisha jiko lako maa baada ya kutumia kuepuka uharibifu na mafuta kugandiana.

Mbali na nyama, kwa kutumia jiko hili unaweza kuchomea mahindi, viazi na chakula chochote kinachofaa kuchomwa.

Kwa wadau wa bidhaa za jikoni, jiko hili linapatikana kwa Sh70,000 hadi Sh100,000 na zaidi.

Kisingizo chako cha kuendelea kutumia mkaa ni nini? Tueleze tukuletee suluhu.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV