Jenista kuzikwa Desemba 16, mkoani Ruvuma

December 12, 2025 12:40 pm · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link
  • Mazishi yake kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Spika wa Bunge, Waziri Mkuu, na Makamu wa Rais.

Dar es Salaam. Mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa Jumanne ya Desemba 16, 2025 katika kijiji cha Ruanda, Mbinga mkoani Ruvuma.

Jenista ambaye amekuwa Mbunge wa Peramiho kwa takribani miaka 25 kwa kuchaguliwa na wananchi na kuteuliwa kwa viti maalumu, amefariki dunia jana Desemba 11, 2025 jijini Dodoma.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Ofisi ya Bunge usiku wa Desemba 11, 2025, leo Desemba 12, 2025, mwili utawasili nyumbani kwa marehemu eneo la Itega, jijini Dodoma ambapo maombolezo yatakuwa yakiendelea.

Aidha, ratiba inaonesha kuwa Jumamosi Desemba 13, kutakuwa na ibada kwenye Kanisa Katoliki Kiwanja cha Ndege, ambapo pia salamu za rambirambi zitatolewa na wananchi watapata fursa ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu na baadaye alasiri safari ya kuelekea Songea itaanza.

Ratiba hiyo inafafanua kuwa, Desemba 14, 2025, mwili utapelekwa Kanisa Katoliki Matogoro, Songea Mjini ambako kutakuwa na ibada, kisha baadaye mwili kupelekwa nyumbani kwa marehemu Makambi, Songea Mjini.

Jumatatu Desemba 15, 2025 asubuhi safari ya kuelekea Peramiho itaanza ambapo ikifuatiwa na ibada, salamu za rambirambi na kuaga mwili, kabla ya siku inayoafuata kuelekea kijijini Ruanda, wilayani Mbinga kwa maziko.

Viongozi mbalimbali wanatarajiwa kuhudhuria shughuli hizo za mazishi akiwemo Spika wa Bunge, Mussa Zungu, Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba na Makamu wa Rais, Dk Emmanuel Nchimbi.

Jenista atakumbukwa kwa bidii yake ya uongozi alipotumika katika nyadhifa mbalimbali ndani ya Serikali ya Tanzania tangu ajihusishe rasmi na masuala ya siasa mwaka 1987

Historia yake iliandikwa kwa kalamu ya wino na kuacha alama katika awamu tatu za Serikali za Tanzania kuanzia ile ya Jakaya Kikwete, John Magufuli hadi awamu ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Kiongozi huyo mashuhuri ambaye pia ni miongoni mwa wanasiasa wakongwe bungeni anafutika katika uso wa dunia wakati ambao bado jimbo la Peramiho linamuhitaji baada ya kumpa ridhaa katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 29 kuliongoza kwa miaka mitano ijayo.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: NDEJEMBI AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI WIZARA YA NISHATI

🔴LIVE: NDEJEMBI AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI WIZARA YA NISHATI

Nukta TV

🔴LIVE: RAIS SAMIA, MAMALISHE,  BABALISHE WANAJAMBO LAO LEO

🔴LIVE: RAIS SAMIA, MAMALISHE, BABALISHE WANAJAMBO LAO LEO

Nukta TV

🔴LIVE: HOTUBA YA BAJETI OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA)

🔴LIVE: HOTUBA YA BAJETI OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA)

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.