Hitilafu mfumo wa malipo yasababisha changamoto manunuzi ya umeme nchini

October 2, 2025 3:24 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Hitilafu hiyo imesababisha huduma zote za ununuzi wa umeme kupitia mitandao ya simu, mawakala na benki kutokuwa na ufanisi.

Dar es Salaam. Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limesema changamoto ya manunuzi ya umeme (LUKU) iliyotokea siku za hivi karibuni imesababishwa na  hitilafu kwenye Mfumo wa Malipo ya Serikali (GePG).

Hali hiyo imesababisha malalamiko miongoni watumiaji wa huduma ya umeme kwa kuwa ndio nishati inayotegemewa kwa kiasi kikubwa kufanikisha shughuli za kiuchumi kama uchakataji wa bidhaa katika viwanda vidogo.

Aidha, wajasiriamali wanaotegemea umeme kuhifadhi bidhaa zao kama mama lishe na wanaouza bidhaa oza (matunda, nyama) watatakiwa kutafuta nishati mbadala ili kuepuka hasara ya kuharibikiwa na bidhaa zao mpaka pale huduma zitakaporejea.

Kwa mujibu wa taarifa ya iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano na Huduma kwa Wateja Tanesco, hitilafu hiyo imesababisha huduma zote za ununuzi wa umeme kupitia mitandao ya simu, mawakala na benki kutokuwa na ufanisi.

“Changamoto hii inasababishwa na hitilafu kwenye mfumo wa malipo ya Serikali (GePG). Tayari  wataalamu wa GePG wanashughulikia changamoto iliyojitokeza ili huduma iweze kurejea katika hali ya kawaida,” imeeleza taarifa hiyo.

Aidha,Tanesco imetoa wito kwa wataalamu wa GePG kushughulikia tatizo hilo kwa haraka ili kuwaondolea wateja usumbufu ikiongeza kuwa itawafahamisha wateja wake pale huduma zitakaporejea kikamilifu.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
7 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
7 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV