Hapana: Ofisi ya Waziri Mkuu haitoi mikopo kwa wananchi

January 9, 2024 9:28 am · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Yasema haitambui kampuni ya Branch Mikopo inayodaiwa kutoa mikopo hiyo kwa udhamini wa Ofisi ya Waziri Mkuu.
  • Yafafanua sehemu sahihi za kupata taarifa za uhakikika kuhusu utolewaji wa mikopo nchini.

Dar es Salaam. Huenda umekutana na matangazo mtandaoni kuwa Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa inatoa mikopo kwa wananchi, taarifa hiyo si ya kweli.

Katika taarifa hiyo ya uzushi kampuni iliyojitambulisha kwa jina la Branch Mikopo Tanzania imekuwa ikitangaza kutoa mikopo mtandaoni chini ya udhamini wa Ofisi ya Waziri Mkuu, jambo ambalo halina ukweli wowote.


Zinazohusiana: Sio kweli: Thabo Mbeki hajafariki dunia


Taarifa rasmi iiliyotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu leo Januari 9, 2024 kupitia ukurasa wa X (zamani Twitter) inafafanua kuwa Ofisi hiyo haitoi mkopo wowote kwa wananchi. 

“Tunapenda kuujulisha umma kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu haiitambui Taasisi hiyo, na wala Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa haitambui na hajawahi thibitisha popote uhalali wa Taasisi hiyo,” imesema taarifa hiyo.

Utaratibu wa kutoa mikopo

Serikali inautaratibu wa kutoa mikopo kwa wananchi kupitia baraza la uwezeshaji wananchi Kiuchumi, mfuko wa maendeleo ya vijana pamoja na mikopo inayotolewa na Halmashauri kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu ulenye ulemavu.

Aina zote za mikopo zinatolewa kupitia mamlaka husika zilizopewa dhamana ya utoaji wa mikopo hiyo, mathalan mikopo ya vikundi vya wanawake,vijana na wenye ulemavu hutolewa katika Halmashauri husika ambazo makundi hayo yanatokea.

Hata baada ya kufika katika mamlaka hizo usajili wote hufanyika ofisini kwa kujaza fomu, kuwasilisha nakala ya katiba ya kikundi, cheti cha usajili wa kikundi, nakala za utambulisho kutoka kwa Mtendaji wa kijiji pamoja na taarifa ya akaunti ya benki ya kikundi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
13 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV