Halmashauri zatakiwa kujenga miradi ya kimkakati kwa mapato ya ndani

September 27, 2019 9:12 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni halmashauri za Mfundi na Mafinga ambazo zinakusanya zaidi ya Sh7 bilioni kwa mwaka.
  • Zimeonywa zisisubiri fedha kutoka Serikali Kuu kutekeleza miradi ya maendeleo. 
  • Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa aendelea kuwabana viongozi wa mkoa wa Iringa. 

Dar es Salaam. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amewataka viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Mufindi na Halmashauri ya Mji wa Mafinga wahakikishe wanajenga mradi wa kimkakati kwa kutumia fedha za mapato ya ndani na si kusubiri miradi kutoka Serikali Kuu. 

Amesema halmashauri hizo zinakusanya zaidi ya Sh7 bilioni saba kwa mwaka, lakini matumizi yake si mazuri kwa sababu hazina mradi wowote wa kimkakati wanaoutekeleza ambao ungewaongezea mapato.

”Nataka kuona mradi wa kimkakati ukitekelezwa kwa fedha mnazokusanya kutoka kwa wananchi,” amesema Majaliwa aliyekuwa akizungumza jana (Septemba 26, 2019) katika mkutano wa hadhara wilayani Mufindi mkoani Iringa.  

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu inaeleza kuwa viongozi hao wanaweza kutenga Sh1 bilioni kwa mwaka na kujenga hospitali au wakatenga fedha na kujenga barabara za lami kwa awamu.


Soma zaidi: 


Amesema ujenzi wa barabara za lami mijini ni Sh300 milioni kwa kilomita moja, hivyo wangeweza kutekeleza ujenzi huo kutokana na fedha wanazokusanya.

“Msitegemee fedha kutoka Serikali Kuu tu jengeni wenyewe barabara zenu kuzunguka Mji wa Mafinga kwa kiwango cha lami kwa sababu mna fedha za kutosha tena mnaweza kutumia fedha za mapato ya ndani mnazokusanya kutoka kwa wananchi badala ya kuzitumia kwa kulipana posho tu,” amesema Majaliwa.  

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
14 Sep, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
14 Sep, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
14 Sep, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Haya ndio maajabu ya iPhone Duo simu mpya kutoka Apple

Haya ndio maajabu ya iPhone Duo simu mpya kutoka Apple

Nukta TV

Kitakachotokea IGP, CDF na DCI wasipofika mahakamani kesi ya Lissu

Kitakachotokea IGP, CDF na DCI wasipofika mahakamani kesi ya Lissu

Nukta TV

Jinsi waajiri wanavyokimbilia 'Interns' kukwepa ajira za kudumu

Jinsi waajiri wanavyokimbilia 'Interns' kukwepa ajira za kudumu

Nukta TV