Fahamu visiwa viwili vinavyoongoza kwa ukubwa Tanzania bara

January 22, 2019 8:30 pm · Zahara
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni visiwa cha Ukerewe kilichopo katika ziwa Victoria pamoja na kisiwa cha Mafia katika bahari ya Hindi.
  • Visiwa hivyo vimezungukwa na vivutio mbalimbali vya utalii ambavyo vikitumika vizuri vitasaidia kukuza sekta ya utalii nchini.

Dar es Salaam. Tanzania ni nchi iliyobarikiwa kuwa na vivutio vingi katika bahari hadi nchi kavu ambavyo vinazidi kuipa thamani nchi hasa kwenye sekta ya Utalii.

Hata hivyo moja ya sehemu zinazovutia watu zaidi ni visiwani ambapo watu wanapata nafasi ya kuvuka maji na kwenda kujionea mandhari ya kuvutia hasa fukwe.

Kwa mujibu wa Ripoti ya Taifa ya Takwimu za Mazingira mwaka 2017-Tanzania Bara inaonyesha visiwa vikubwa viwili ambavyo ni Kisiwa cha Ukerewe chenye kilometa za mraba 647 kilichopo Katika Ziwa Victoria.

Huku cha pili ni kisiwa cha Mafia kilichopo katika Bahari ya Hindi chenye Kilomita za mraba 518. Visiwa hivi ni asilimia 0.12 ya ardhi iliyopo nchini Tanzania.

Maeneo haya yote yamebarikiwa kuwa na hali ya hewa nzuri na vivutio mbalimbali vya utalii vinavyofanya watalii kwenda kujionea kama vile fukwe, mazingira na maeneo mbalimbali ya historia.

​

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV