Facebook, Instagram ‘kufichua’ kiwango cha muda unaotumika mtandaoni

August 28, 2018 1:08 pm · TULINAGWE ALSON
Share
Tweet
Copy Link
  •  Ni mabadiliko ya hivi karibuni yanayohusisha mitandao ya kijamii.
  • Yatahusisha kujua muda unaotumika kwenye mitandao hiyo.

Dar es Salaam. Mitandao ya kijamii ni moja ya vitu vinavyounganisha watu kutoka sehemu mbalimbali na kufanya dunia kuwa kijiji.

Kutokana na kasi ya matumizi ya mitandao ya kijamii, kampuni zinazotoa huduma hizo hufanya maboresho ya teknolojia ili kuhakikisha wanaendelea kubaki katika soko laushindani.

 Mitandao ya Facebook na Instagram imetangaza kufanya maboresho ambayo yatawawezesha watumiaji kujua muda wanaotumia wakiwa katika mitandao hiyo.

Huduma hiyo mpya itasaidia kujua au kutathmini matumizi ya mitandao kila siku  ambapo mtumiaji ataweza kudhibiti muda anaoingia na kutoka kwenye mitandao hiyo. Huduma hiyo inapatikana kwenye kipengele kinachojulikana kama “Activity Dashboard”. 

Pia kuna namna ambavyo mtu anaweza kuseti kiwango cha muda kwa siku na kukumbushwa pale muda unapokua umefika ili kumuachisha na uteja wa kutumia mitandao. 

Mabadiliko hayo, ambayo yamefanywa na Facebook na Instagram yataanza hivi karibuni, pia yatawawezesha watumiaji kudhibiti kiwango cha taarifa zinazowafikia mara kwa mara (notifications). 

Facebook na Instagram zinazomilikia na Bilionea Mark Zuckerberg, zimefanya maboresha hayo ikiwa ni sehemu ya kuwa karibu na wateja wao. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV