Facebook, Instagram ‘kufichua’ kiwango cha muda unaotumika mtandaoni
- Ni mabadiliko ya hivi karibuni yanayohusisha mitandao ya kijamii.
- Yatahusisha kujua muda unaotumika kwenye mitandao hiyo.
Dar es Salaam. Mitandao ya kijamii ni moja ya vitu vinavyounganisha watu kutoka sehemu mbalimbali na kufanya dunia kuwa kijiji.
Kutokana na kasi ya matumizi ya mitandao ya kijamii, kampuni zinazotoa huduma hizo hufanya maboresho ya teknolojia ili kuhakikisha wanaendelea kubaki katika soko laushindani.
Mitandao ya Facebook na Instagram imetangaza kufanya maboresho ambayo yatawawezesha watumiaji kujua muda wanaotumia wakiwa katika mitandao hiyo.
Huduma hiyo mpya itasaidia kujua au kutathmini matumizi ya mitandao kila siku ambapo mtumiaji ataweza kudhibiti muda anaoingia na kutoka kwenye mitandao hiyo. Huduma hiyo inapatikana kwenye kipengele kinachojulikana kama “Activity Dashboard”.

Pia kuna namna ambavyo mtu anaweza kuseti kiwango cha muda kwa siku na kukumbushwa pale muda unapokua umefika ili kumuachisha na uteja wa kutumia mitandao.
Mabadiliko hayo, ambayo yamefanywa na Facebook na Instagram yataanza hivi karibuni, pia yatawawezesha watumiaji kudhibiti kiwango cha taarifa zinazowafikia mara kwa mara (notifications).
Facebook na Instagram zinazomilikia na Bilionea Mark Zuckerberg, zimefanya maboresha hayo ikiwa ni sehemu ya kuwa karibu na wateja wao.