COSTECH yafungua milango kwa wabunifu kufaidika kiuchumi

August 16, 2018 7:10 pm · Daniel
Share
Tweet
Copy Link
  • Mbunifu awe na wazo linaloweza kutatua changamoto za jamii inayomzunguka.
  • Watakaofanikiwa kupata Sh40 milioni kuendesha miradi yao.

Dar es salaam. Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa kushirikiana na Mfuko wa Ubunifu wa Maendeleo ya Watu (HDIF) wanakusudia kuanzisha mradi kuwajengewa uwezo wajasiriamali kubuni miradi itakayochochea ukuaji wa uchumi nchini.

Mradi huo uliopewa jina la “Fursa ya Kukuza Ubunifu” utawahusu wajasiriamali. wabunifu na watafiti, ambao watapatikana kupitia ushindani wa maandiko ya miradi inayolenga kuimarisha mfumo wa ubunifu nchini kupitia tafiti zinazolenga kutatua changamoto zilizopo katika jamii. 

Wajasiriamali ambao mawazo yao yatakubalika watapata mitaji ya kuendesha shughuli zao ili kuboresha maisha ya jamii zinazowazunguka. Kigezo cha kupata ufadhili huo ni kuwa na mawazo ya kibunifu yaliyowekwa kwenye maandishi yakielezea tatizo, njia ya kutatua, matokeo tarajiwa, mgawanyo majukumu na ufanisi wa timu ya watu ambao watatekeleza wazo husika.

”Kusudio la ubunifu ni  kutoa msaada wa kifedha katika kuendeleza ubunifu ambao utachangia maendeleo ya kiuchumi na kijamii hapa Tanzania,” inaeleza sehemu ya taarifa ya COSTECH ambayo inawataka wajasiriamali wenye nia ya kupata mtaji wawasilishe maandiko yao mpaka Septemba 9 mwaka huu. 

Watu ambao wanaweza kuingia kwenye mradi huo ni watu binafsi wenye mawazo ya mabadiliko, taasisi au mashirika yanayotengeneza bidhaa au kutumia teknolojia kuendeleza ubunifu katika jamii.  Wajasiriamali 15 ambao mawazo au maandiko yao yatathibitika kukidhi vigezo watapata ruzuku ya kuendesha miradi yao yenye thamani Sh40 milioni kwa kila mradi.

Mradi huo unakusudia kufanywa kwa mwaka mmoja ambao utagawanywa katika makundi matatu ya watafiti ambao wanatakiwa wawe wanne, wabunifu (4) na kundi la mwisho ni watafiti na wajasiriamali ambao watakuwa saba.

Utekelezaji wa mradi huo ni sehemu ya  jitihada za ndani na nje ya nchi zinazofanywa na mashirika mbalimbali katika kukuza ubunifu na ujasiriamali nchini katika sekta za afya, elimu, kilimo na teknolojia.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV