Corona yashusha bei magari yanayotumia umeme

May 28, 2020 9:23 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Kampuni inayotengeneza magari hayo ya Tesla imesema itashusha bei ili kuvutia wateja wengi zaidi.
  • Imesema janga la Corona limeathiri manunuzi ya magari hayo. 

Kampuni ya Tesla inayotengeneza magari ya umeme imesema itapunguza bei ya baadhi ya magari hayo ili kuvutiwa wateja wengi kwa sababu mahitaji yameanza kushuka kutokana na athari za janga la Corona. 

Kampuni hiyo imesema punguzo hilo la bei litazifaidisha nchi za China na zile za bara la Amerika Kaskazini kwa magari aina ya Model 3, S na X n alitakuwa kati ya asilimia 4 hadi asilimia 6. 

Tesla imeeleza katika taarifa yake kuwa athari za janga la Corona limechangia kuongezeka kwa ukosefu wa ajira na kuathiri kipato cha watu wengi duniani, hivyo wameamua kupunguza bei ya magari ili kuvutia wateja.


Zinazohusiana:


Tesla inategemea kuuza magari 500,000 yanayotumia umeme mwaka huu lakini itategemeana mwenendo wa uchumi wa dunia ambao umeathiriwa na Corona. 

Magari ya umeme yamekuwa yakipigiwa chepuo na watetezi wa mazingira kwa sababu ni njia mojawapo ya kulinda mazingira hasa kupunguza uchafuzi wa hewa. 

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mikakati ya Serikali kuhakikisha walimu wa VETA wanapata ajira na mikopo

Mikakati ya Serikali kuhakikisha walimu wa VETA wanapata ajira na mikopo

Nukta TV

Mama Salama alivyombana Wanu kuhusu maslahi ya walimu wanaojitolea

Mama Salama alivyombana Wanu kuhusu maslahi ya walimu wanaojitolea

Nukta TV

Kwanini uchafuzi wa mazingira ni tishio kwa afya ya binadamu na uchumi

Kwanini uchafuzi wa mazingira ni tishio kwa afya ya binadamu na uchumi

Nukta TV