Bei ya viazi mviringo haikamatiki Lindi

March 20, 2020 12:27 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Bei inayotumika leo Lindi ni mara nne zaidi ya Njombe, jambo linalowafaidisha zaidi wafanyabiashara ambao wamepeleka viazi mviringo mkoani humo. 
  • Gunia la kilo 100 la viazi mviringo katika masoko ya mkoani Lindi  linauzwa kwa Sh120,000, wakati masoko ya Njombe linauzwa kwa Sh30,000.

Dar es Salaam. Watumiaji wa viazi mviringo hasa kutengeneza chipsi katika Mkoa wa Lindi leo watalala na maumivu kutokana na bei ya gunia la kilo 100 la zao hilo kuuzwa mara nne zaidi ya bei inayotumika katika Mkoa wa Njombe. 

Takwimu za mazao makuu ya chakula zilizotolewa na WIzara ya Viwanda na Biashara  leo (Machi 20, 2020) zinaeleza kuwa gunia la kilo 100 la viazi mviringo katika masoko ya mkoani Lindi  linauzwa kwa Sh120,000, wakati masoko ya Njombe linauzwa kwa Sh30,000.

Hiyo ina maana kuwa bei inayotumika leo Lindi ni mara nne zaidi ya Njombe, jambo linalowafaidisha zaidi wafanyabiashara ambao wamepeleka viazi mviringo mkoani humo. 

Bei hiyo inayotumika Lindi ndiyo bei ya juu huku ya Njombe ikiwa ni ya chini ikilinganishwa na bei zinazotumika katika maeneo mengine nchini.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV