ATCL kuanza safari za kwenda Mumbai, India leo

July 17, 2019 5:02 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Kwa mujibu wa shirika hilo, safari kwanza itakuwa leo (Julai 17, 2019) na ya pili itakua Juali 19 kwenda moja kwa moja Mumbai.

Dar es Salaam. Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) leo linaanza safari ya kwenda katika jiji la Mumbai nchini India ikiwa ni hatua muhimu ya shirika hilo la umma kujitanua katika utoaji wa huduma za usafiri wa anga kimataifa. 

Safari hiyo mpya inakuja ikiwa zimepita zaidi ya wiki mbili tangu ATCL ilipozindua safari zake kutoka Tanzania hadi katika jiji la Johannesburg nchini Afrika Kusini

Kwa mujibu wa shirika hilo, safari kwanza itakuwa leo (Julai 17, 2019) na ya pili itakua Juali 19 kwenda moja kwa moja Mumbai. 

“Tunafurahi kutangaza kwamba safari yetu ya kwanza tarehe 17 kwenda Mumbai na ya Pili tarehe 19 Julai 2019 tutatumia uwanja mpya wa Julius Nyerere wa safari za kimataifa Terminal 3,” unasomeka ujumbe uliowekwa katika ukurasa wa Twitter wa ATCL.

Kwa anayetaka kusafiri hadi Mumbai, sasa atalipa dola za Marekani 378 sawa na takriban Sh869,232.

Hata hivyo, ATCL itakuwa na kibarua kigumu cha kuboresha huduma zake na kujiimarisha ili kuhimili ushindani wa mashirika makubwa ya Kenya Airways na Ethiopia Airlines ambayo yametawala soko la usafiri wa anga Afrika.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV