ATCL kuanza safari za kwenda Mumbai, India leo
- Kwa mujibu wa shirika hilo, safari kwanza itakuwa leo (Julai 17, 2019) na ya pili itakua Juali 19 kwenda moja kwa moja Mumbai.
Dar es Salaam. Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) leo linaanza safari ya kwenda katika jiji la Mumbai nchini India ikiwa ni hatua muhimu ya shirika hilo la umma kujitanua katika utoaji wa huduma za usafiri wa anga kimataifa.
Safari hiyo mpya inakuja ikiwa zimepita zaidi ya wiki mbili tangu ATCL ilipozindua safari zake kutoka Tanzania hadi katika jiji la Johannesburg nchini Afrika Kusini.
Kwa mujibu wa shirika hilo, safari kwanza itakuwa leo (Julai 17, 2019) na ya pili itakua Juali 19 kwenda moja kwa moja Mumbai.
“Tunafurahi kutangaza kwamba safari yetu ya kwanza tarehe 17 kwenda Mumbai na ya Pili tarehe 19 Julai 2019 tutatumia uwanja mpya wa Julius Nyerere wa safari za kimataifa Terminal 3,” unasomeka ujumbe uliowekwa katika ukurasa wa Twitter wa ATCL.
Excited and Ready For Mumbai, only a few hours left.#FlyAirTanzania
#thewingsofkilimanjaro#AirTanzania
#mumbai#india
pic.twitter.com/MVLBHvmn2W— Air Tanzania (@AirTanzania) July 17, 2019
Kwa anayetaka kusafiri hadi Mumbai, sasa atalipa dola za Marekani 378 sawa na takriban Sh869,232.
Hata hivyo, ATCL itakuwa na kibarua kigumu cha kuboresha huduma zake na kujiimarisha ili kuhimili ushindani wa mashirika makubwa ya Kenya Airways na Ethiopia Airlines ambayo yametawala soko la usafiri wa anga Afrika.
Latest