Aliyekuwa RC Simiyu apandishwa kizimbani Mwanza kwa mara ya kwanza

July 9, 2024 1:47 pm · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link
  • Nawanda amepandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza tangu jeshi la polisi mkoani Mwanza litangaze kumtia nguvuni Juni 13 mwaka huu.
  • Hata hivyo mtuhumiwa amekana kosa na kesi hiyo itasikilizwa tena Julai 16 mwaka huu.

Mwanza. Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Yahaya Nawanda, amefikishwa katika Mahakama ya  Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza na kusomewa shitaka moja la kumwingilia kinyume na maumbile Tumsiime Ngemela (21) katika eneo la Rock City mall jijini Mwanza.

Mshitakiwa huyo amefikishwa katika mahakama hiyo mapema leo Julai 9, 2024 na kusomewa shitaka hilo ambalo anadaiwa kulitenda Juni 2, 2024  kinyume na kifungu cha 154 (a) cha Kanuni ya Adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2022

Waendesha mashitaka wa kesi hiyo ambao ni Wakili wa Werikali Magreth Mwaseba na Martha Mtiti waliitaja kesi hiyo kuwa ni kesi namba 1883 ya mwaka 2024 mbele ya Erick Maley, Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo.

Hata hivyo mshtakiwa alikana shitaka hilo na yuko nje kwa dhamana baada ya kukamilisha masharti aliyokuwa amewekewa ambayo ni kuwa mtumishi wa Serikali pamoja na bondi  ya mali isiyohamishika yenye thamani ya Sh5 milioni.

Mshtakiwa atakuwa nje kwa dhamana hadi Julai 16, 2024 ambapo kesi hiyo itaanza kusikilizwa kwa hoja za awali huku upande wa mlalamikaji ukitakiwa kupeleka mashahidi.

Akizungumza nje ya mahakama, Wakili wa upande wa utetezi, Constantine Mtalemwa amesema kwa sasa wanaiachia mahakama namna itakavyoendeshwa kesi hiyo na kwamba kesi ni ya wazi hivyo watanzania  wote wanaruhusiwa kuifuatilia.

“Jambo linapokuja mahakamani tunaiachia mahakama  hatuwezi kuanza kuongelea ushahidi kwa kuwa kesi haijaanza  na wananchi wanakaribishwa kuja kusikiliza kwakuwa ni kesi ya wazi,” amesema Mtalemwa.

Mshitakiwa  huyo anapandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza ikiwa ni ni takribani wiki tatu tangu akamatwe na kufikishwa kituo kikuu cha polisi cha wilaya ya Nyamagana Juni 13 mwaka huu.


Soma zaidi: Rais Samia: Tunahitaji mapato ili tupunguze kukopa


Alivyoingia mahakamani

Mshitakiwa huyo aliingia mahakamani majira ya saa 4.00 asubuhi akitumia  gari aina ya Toyota landcruiser huku akiwa amezungukwa na ulinzi mkali wa polisi ukiongozwa na Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Mwanza Saudi Yessaya.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
9 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
9 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Ulinzi waimarishwa Dar, maduka yachelewa kufunguliwa

Ulinzi waimarishwa Dar, maduka yachelewa kufunguliwa

Nukta TV

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV