Dola yapungua kwa Sh10 NMB, Euro na Pauni zapanda CRDB
- Wanunuaji wa sarafu hiyo kupitia benki ya NMB watanunua dola kwa bei nafuu zaidi kulinganisha na jana.
Dar es Salaam. Dola ya Marekani imepungua kwa Sh10 katika Benki ya NMB, ikilinganishwa na jana, wakati Benki ya CRDB imeendelea kubakiza viwango vyake bila mabadiliko.
Takwimu za viwango vya ubadilishaji fedha zinaonyesha NMB sasa inanunua Dola ya Marekani (USD) kwa Sh2,595 kutoka Sh2,605 jana na kuiuza kwa Sh2,675 kutoka Sh2,685.
Kwa upande wa CRDB, dola imeendelea kununuliwa kwa Sh2,605 na kuuzwa kwa Sh2,685, viwango vilivyodumu kwa siku mbili mfululizo.
Hii inamaanisha kuwa wanunuaji wa sarafu hiyo kupitia benki ya NMB watanunua dola kwa bei nafuu zaidi kulinganisha na jana.
Wakati dola ikipungua NMB, Euro (EUR) imeendelea kuimarika zaidi katika CRDB. Benki hiyo imeongeza kiwango cha ununuzi kwa Sh9.86 hadi Sh2,904.69 kutoka Sh2,894.83, huku bei ya uuzaji ikipanda hadi Sh3,204.69 kutoka Sh3,194.83.

NMB, kwa upande wake, imepunguza bei ya uuzaji wa euro kwa Sh5 hadi Sh3,177 kutoka Sh3,182 na kushusha bei ya ununuzi kwa Sh5 hadi Sh2,904 kutoka Sh2,909.
Pauni ya Uingereza (GBP) nayo imeonyesha mwelekeo unaofanana. CRDB imeongeza kiwango cha ununuzi kwa Sh7.81 hadi Sh3,412.30 na uuzaji hadi Sh3,712.30, wakati NMB imepunguza viwango vyake kwa Sh8 na sasa inanunua pauni kwa Sh3,359 na kuiuza kwa Sh3,704.
Kwa upande sarafu za kikanda, Shilingi ya Kenya (KES) imeendelea kubaki katika viwango vya jana CRDB, lakini NMB imepunguza bei yake kidogo kutoka Sh17.9 hadi Sh17.8 kwa ununuzi na kutoka Sh22.5 hadi Sh22.4 kwa uuzaji. Shilingi ya Uganda (UGX) imeendelea kubaki katika viwango vya jana katika benki zote mbili.