Euro, Pound zaimarika dola yabaki tulivu Agosti 10, 2026
- Watumiaji wa dola wataendelea kununua dola kwa bei sawa na wiki iliyopita.
Dar es Salaam. Euro na Pound zaimarika dola ya Marekani ikibaki katika viwango vilevile katika benki za CRDB na NMB ikilinganishwa na mwisho wa wiki iliyopita.
Kwa mujibu wa viwango vya ubadilishaji fedha katika benki za CRDB Bank na NMB, dola ya Marekani imeendelea kununuliwa kwa Sh2,605 katika CRDB na Sh2,595 NMB, huku ikiuzwa kwa Sh2,685 na Sh2,675 mtawalia katika benki hizo.
Hata hivyo, Euro imepanda katika benki zote mbili. CRDB inanunua Euro moja kwa Sh2,912 kutoka Sh2,904.39 Ijumaa, huku bei ya kuuza ikifikia Sh3,212 kutoka Sh3,204.39.
NMB nayo inanunua Euro kwa Sh2,910 kutoka Sh2,902, wakati bei ya kuuza imeongezeka hadi Sh3,183 kutoka Sh3,176.

Pound ya Uingereza (Sterling) pia imeimarika. CRDB inanunua Pound kwa Sh3,423 kutoka Sh3,414.18 na kuuza kwa Sh3,723 kutoka Sh3,714.18.
Kwa NMB, Pound imenunuliwa kwa Sh3,365 kutoka Sh3,359, huku bei ya kuuza ikipanda hadi Sh3,741 kutoka Sh3,704.
Kwa upande wa sarafu za kikanda Shilingi ya Kenya, CRDB imeendelea na viwango vilevile vya Sh16.96 kwa ununuzi na Sh23.96 kwa uuzaji. NMB imeongeza bei ya kununua kutoka Sh17.80 hadi Sh17.90, huku bei ya kuuza ikibaki Sh22.50.