Zege Ndizi: aina mpya ya msosi inayovutia wengi

August 2, 2024 11:25 am · Mlelwa Kiwale
Share
Tweet
Copy Link
  • Maandalizi yake hayatofautiani sana na chipsi zege
  • Unaweza kutumia aina yoyote ya ndizi unayopendelea

Si watoto wala watu wazima wasiofahamu kuhusu chipsi zege hapa nchini kwetu.

Urahisi wa kuandaa na ladha yake ndiyo kivutio kikuu kwa watu wengi kuchagua msosi huu pale wanapotembelea hotelini na sehemu nyingine zinazouzwa chakula.

Vipi leo nikikutonya kuwa unaweza kuandaa zege kivingine kwa kutumia ndizi mbivu au mbichi?

Usijiulize sana jikopoint leo imekuletea mapishi rahisi ya ndizi zege unazoweza kuandaa nyumbani au katika sehemu yako ya biashara.

Maandalizi 

Hatua ya kwanza ni kuchagua aina ya ndizi unaozitaka kutumia au zinazopatikana kwa urahisi katika eneo lako, iwe ni mzuzu,bukoba au malindi zote zinaweza kufaa katika aina hii ya mapishi.

Anza mapishi yako kwa kumenya ndizi na uzikate katika vipande vidogo vidogo itapendeza zaidi kama utakata umbo la duara kisha uvioshe na uendee kuandaa viungo vingine kama kitunguu, karoti na hoho.

Ukimaliza chuja maji kwenye ndizi hakikisha zimekauka kabla ya kuwasha jiko na kuzikaanga mpaka ziwe na rangi ya kahawia ndio utoe na kuchuja mafuta.

Rudia hatua hiyo mpaka ndizi zote ulizoziandaa ziishe kisha hamia kwenye kuandaa zege.

Hatua hii inafanana kabisa na Ile ya chipsi zege, cha kufanya ni kupasua mayai na kuyakoroga mpaka yachanganyike vizuri.

Ongeza viungo kaka hoho, karoti, vitunguu, chumvi na pilipili manga kama unapendelea kisha uendelee na hatua ya kukaanga ambapo utaanza kwa kuweka ndizi katika kikaangio (frying pan) kisha utamimina mayai na kuyasambaza yaenee katika kikaangio chote.

Baada ya kumimina utasubiri mpaka upande wa pili uive ndio utageuza  na baada ya dakika kama tatu au nne utageuza tena kuangalia kama pande zote zimeiva.

Wakati wote wa mapishi ya msosi huu hakikisha unapika kwa wastani ili ndizi pamoja na mayai yaive vizuri.

Ukiona ndizi zege imeanza kupata rangi ya kahawia hapo itakuwa tayari kwa kuliwa ikisindikizwa na kachumbari, mbogamboga na hata soda.

Kama ilivyo kwa chipsi zege, msosi huu pia unaweza kutumiwa muda wowote iwe asubuhi, mchana au jioni.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV