Uwekezaji wa kigeni Tanzania waongezeka kwa asilimia 0.4 mwaka 2024

Tanzania imeendelea kushuhudia ukuaji wa uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nje ya nchi (FDI) katika kipindi cha miaka minne kuanzia mwaka 2020 hadi 2024, huku thamani ya uwekezaji huo ikifikia Dola za Marekani milioni 1,656 mwaka 2024.
Takwimu zinaonyesha kuwa kiwango hicho ni ongezeko la asilimia 0.4 kutoka Dola milioni 1,648.9 zilizorekodiwa mwaka 2023.
Hata hivyo, ongezeko hilo ni dogo zaidi kuwahi kurekodiwa ndani ya kipindi hicho cha miaka mitano.
Mwaka 2020 Tanzania ilirekodi Dola za Marekani milioni 943.8 za uwekezaji kutoka nje, kabla ya kuongezeka hadi Dola milioni 1,190.5 mwaka 2021 na kufikia Dola milioni 1,437.6 mwaka 2022.