Rais Samia amteua Mcheche Masaju kuwa Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania
June 13, 2025 10:10 am ·
Esau Ng'umbi
Dar es Salaam. Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amemteua Jaji wa Mahakama ya Rufani George Masaju kuwa Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania kuchukua nafasi ya Prof Ibrahim Hamis Juma ambaye amestaafu baada ya kuhudumia mhimili huo wa dola kwa miaka minane.
Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu leo Juni 13, imebainisha kuwa uapisho wa Masaju utafanyika Juni 15, 2025 Ikulu, Chamwino Dodoma.
Kabla ya kuteuliwa kushika nafasi hiyo Jaji Masaju amewahi kuwa mshauri wa Rais Jakaya Kikwete katika masuala ya kisheria na baadae alihudumu kama Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Januari 22, mwaka huu Jaji Masaju aliapishwa na Rais Samia kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani
Latest

3 hours ago
·
Kelvin Makwinya
Namna Tanzania inavyotaka kulinda viwanda vya ndani bajeti 2025/26

1 day ago
·
Fatuma Hussein
Serikali, wadau wa maendeleo wazindua kampeni ya Pika Smart

1 day ago
·
Kelvin Makwinya
Viwango vya fedha Juni 13, 2025

2 days ago
·
Nuzulack Dausen
Serikali ya Tanzania yapendekeza bajeti Sh56.49 trilioni 2025