Rais Samia apitisha miswada saba kuwa sheria

April 8, 2025 4:28 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni pamoja na Mswada wa Sheria wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) wa mwaka 2024. 

Dar es Salaam. Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, amepitisha miswada saba iliyopitishwa na Bunge katika Mkutano wa 18 wa Bunge la 12 kuwa sheria rasmi za nchi, hatua inayolenga kuimarisha utendaji wa taasisi mbalimbali na kuboresha huduma kwa wananchi.

Akiwasilisha taarifa ya Spika kuhusu kazi zilizokamilika katika mkutano uliopita, leo Aprili 8, 2025 wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 19 wa Bunge, Naibu Spika wa Bunge, Mussa Azzan Zungu ameliarifu Bunge kuwa tayari miswada hiyo saba imesainiwa na Rais na sasa inatambuliwa rasmi kama sheria.

“Napenda kuliarifu Bunge hili tukufu kuwa miswada hiyo saba imepata kibali cha mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa sheria za nchi” amesema Zungu.

Moja ya miswada iliyopitishwa na kusainiwa kuwa sheria ni pamoja na Mswada wa Sheria wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) wa Mwaka 2024 uliolenga kuliwezesha shirika hilo kukabiliana na changamoto za kifedha, kiutendaji, na kiteknolojia ambazo zimekuwa zikilikabili kwa miaka mingi. 

Muswada huo ambao kwa sasa ni sheria unaipa TBC msingi thabiti wa kisheria na kuiwezesha kufanya kazi kwa ufanisi zaidi kwa kuzingatia mahitaji ya kisasa na mabadiliko ya teknolojia.

Kwa mujibu wa maelezo aliyoyatoa Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Prof. Palamagamba Kabudi, kabla muswada huo haujapitishwa na kuwa sheria alisema kuwa sheria hiyo itatambua TBC kama shirika muhimu la umma linalohusika na utangazaji wa habari, burudani, na elimu. 

Pia itaipa mamlaka ya kusimamia rasilimali zake na kuhakikisha kuwa inaendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.

Miswada mingine iliyopitishwa na kuwa sheria ni pamoja na Mswada wa Sheria wa Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. 3 wa Mwaka 2024, Mswada wa Sheria wa Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. 4 wa Mwaka 2024, Mswada wa Sheria wa Marekebisho ya Sheria za Kazi wa Mwaka 2024, Mswada wa Sheria wa Marekebisho ya Sheria ya Usimamizi wa Mazingira wa Mwaka 2024, Mswada wa Sheria wa Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi wa Mwaka 2024, na Mswada wa Sheria ya Kuidhinisha Matumizi ya Nyongeza ya Fedha za Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025.

Upitishwaji wa miswada hiyo saba unatarajiwa kuleta tija kubwa kwa taifa kwa ujumla. Sheria mpya na zilizoboreshwa zitasaidia kuimarisha mazingira ya kazi, kulinda mazingira, kuvutia uwekezaji zaidi kupitia maeneo maalum ya kiuchumi, na kuongeza uwazi na uwajibikaji katika matumizi ya fedha za umma.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
13 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV