TBS: Uivishaji wa ndizi kwa kemikali ya ethylene hauna madhara 

October 16, 2024 11:17 am · Mlelwa Kiwale
Share
Tweet
Copy Link

  • Kemikali hiyo inaruhusiwa kwa matumizi hayo ya kuivisha matunda.
  • Teknolojia hii imepunguza kwa kiasi kikubwa hasara iliyokuwa inajitokeza wakati wa usafirishaji wa matunda.

Dar es Salaam. Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limewataka Watanzania kutokuwa na shaka na afya zao baada ya kula ndizi zilizoivishwa kwa kemikali ya ‘ethylene’ kwa kuwa haina madhara.

Hivi karibuni kuliibuka mijadala kuhusu usalama wa afya za Watanzania baada ya baadhi ya wafanyabiashara jijini Dar es Salaam kukiri kutumia kemikali hiyo kuivisha ndizi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa TBS kupitia kwa Meneja wa Uhusiano na Masoko, Gladness Kaseka Oktoba 13, 2024 utaratibu wa kutumia kemikali kuivisha matunda ni wa kawaida na hutumika duniani kote kwa kuwa husaidia kupunguza gharama na upotevu wa chakula.

“TBS inapenda kuufahamisha umma kuwa teknolojia inayotumika kuivisha matunda kwa kutumia kemikali ya ethylene ni utaratibu wa kawaida unaotumika duniani kote na hauna madhara yoyote kiafya. Aidha, kemikali inayotumika ya ethylene imefanyiwa uchunguzi wa kitaalam juu ya usalama wake na inaruhusiwa kwa matumizi hayo ya kuivisha matunda,” imebainisha taarifa na TBS.

TBS imeongeza kuwa teknolojia hiyo imesaidia kupunguza hasara ilivyokuwa ikijitokeza wakati wa usafirishaji wa matunda yalioiva kwa kuwa imewezesha wafanyabiashara kununua/ kusafirisha matunda yaliyokomaa na kuyaivisha kwa wakati mmoja na kwa kiwango sawa.

Aidha, teknolojia hiyo husaidia ndizi hizo kutokuharibika katika kipindi cha muda mrefu zaidi, ikilinganishwa na zile zilizoivishwa kwa njia ya asili ambayo matunda hutoa gesi asilia ya ‘ethylene’ ili kuiva.

Hata hivyo, TBS imesisitiza kuwa inaendelea kulinda usalama na ubora wa bidhaa zote wakati wote.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV